PRESS
SECRETARY TO THE PRESIDENT
OF
THE UNITED

The State House,
Tel:
Fax. No. 255-22 2113425 DAR ES SALAAM.
E-mail: press@ikulu.go.tz Tanzania.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Premi Kibanga,
Maswa, Shinyanga,
26.Aug, 07
Serikali imetenga Tshs 950 milioni kwa ajili ya kukarabati
bwawa la maji la Niusola wilayani Maswa ili kuwarejeshea
haraka wananchi huduma ya maji
kutokana na bwawa
“Tulitoa ahadi wakati
wa kampeni kwamba tutaimarisha huduma za maji
wilayani hapa, tumeshaanza lakini kwa bahati mbaya
mvua zimebomoa bwawa, hata hivyo
tutalijenga na kurudisha huduma ya maji na kuiboresha zaidi ili wananchi
wengi wapate maji salama” Rais
amesema.
Kubomoka kwa bwawa
Rais Jakaya Kikwete ametembelea Bwawa
Mbali na
Serikali pia imetoa Tsh
milioni 75.42 kwa Halmashauri kwa ajili ya kutoa
huduma za haraka kwa wananchi
kwa kujenga visima vifupi kumi
na moja ambavyo
vitatoa huduma ya maji kwenye
shule za sekondari, huku kukiwa na mpango
mkubwa wa kusambaza maji safi na salama
wilayani kote.
Katika kutekeleza ilani ya uchaguzi ya
CCM ya kuhakikisha watoto wote wenye
umri wa
kwenda shule wanapata nafasi kutoka elimu ya
awali hadi chuo kikuu, Rais
ameelezea kufurahishwa kwake kwa wananchi
kuitikia wito wa kujenga shule
na kuhakikisha kila kata ina
sekondari angalau moja.
Wilaya ya Maswa,
Rais ameingia wilaya ya Maswa
akitokea wilaya ya Meatu ambako
nako alitembelea miradi mbalimbali ya Maji.
“Tunao mpango wa kupunguza matatizo ya maji
na hatimaye kumaliza kabisa tatizo hili la maji
Akiwa katika wilaya hizi mbili
Rais, ameelezea azma ya serikali
ya kuongeza tija katika kilimo.
“Serikali itatoa ruzuku kwa
wakulima ili walime vizuri zaidi,
tutaajiri wataalamu na wasomi wapatao
elfu mbili mia tano (2500) na kuwapeleka katika
kila tarafa” Rais amesema.
Ahadi zingine ambazo ziko katika hatua
ya kati ni kutengeneza barabara katika wilaya za mkoa
huu wa Shinyanga
ambazo zitaunganisha mkoa na mikoa
mingine jirani.
Akiwa Mkoani Shinyanga Rais anaendelea kusisitiza na
kuwahamasisha wananchi kuwa makini na
kuchukua tahadhari kubwa kuepukana na ugonjwa wa
Ukimwi.
Rais ataondoka Maswa tarehe 27 Agosti, 2007 kuelekea wilaya ya Bariadi ambapo
pia anatarajiwa kuzindua bwawa la maji na baadaye kufungua kiwanda cha kuchambulia pamba na kuongea
na wananchi.
Rais yuko Mkoani Shinyanga
kufuatilia na
kuangalia shughuli mbalimbali za wananchi
na kufuatilia kwa karibu utekelezaji
wa ilani ya CCM
Mwisho.