PRESS SECRETARY TO THE PRESIDENT

OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

 

 

 

 

                                                      

                                           The State House,

Tel: 255-22-2116539/2116913                                                    P.O. Box 9120,

Fax. No. 255-22 2113425                                                           DAR ES SALAAM.

E-mail:  press@ikulu.go.tz                                                           Tanzania.

              ikulupress@yahoo.com

 

 

 

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

 

 

Premi Kibanga

Shinyanga.

 

29 Agosti, 2007

 

 

Serikali imeahidi kufanya kila iwezalo kuhakikisha zao la  Pamba halianguki.  Rais amewaambia viongozi wa Mkoa wa Shinyanga leo wakati wa kikao cha majumuisho ya ziara yake ya kikazi ya siku nane moani humo.

 

“Lakini katika kuhakikisha zao hili halianguki, nawategemea nyie viongozi na mipango yenu”  Rais amesema.

 

Akiwapa changamoto wenye viwanda mbalimbali vya kusafirisha  pamba  nje ya nchi na kutengeneza mafuta alisema “Muende mbali zaidi, mzalishe nyuzi na hatimaye nguo ili kuongeza thamani ya pamba yetu”. Mkoa wa Shinyanga unazalisha asilimia 60 ya pamba yote nchini. 

 

Akizungumzia kuhusu sekta nyingine muhimu kwa uchumi wa mkoa wa Shinyanga, Rais ameahidi kwamba sekta ya mifugo itafanyiwa mageuzi ili kuzalisha nyama kwa wingi, maziwa na ngozi bora ili kukuza mapato kwa wafugaji na taifa.

 

Amewahimiza viongozi wa mkoa huo kushirikana na wafugaji kuboresha huduma kwa mifugo kama chanjo, tiba majosho na masoko ya uhakika.

 

Kuhusu sekta ya kilimo, Rais amesema “Tuna nia ya kuongeza matumizi ya maji, kuanzisha programu ya umwagiliaji, kutumia mbegu bora na mbolea ambapo serikali inatoa ruzuku na inafanya jitihada ili ruzuku hiyo iende  kwenye mbolea moja kwa moja”.  Akawataka wakulima kuzingatia kanuni bora za kilimo.

 

Aidha Rais amebainisha kuwa Serikali itaajiri maafisa ugani 2500 waliohitimu elimu ya Chuo Kikuu ambao watapelekwa katika  kila kata na tarafa kwa lengo la kutilia mkazo kilimo na kukiongezea thamani. 

 

Sambamba na kuajiri maafisa ugani hao, Serikali pia itaimarisha miundo mbinu, hasa barabara za vijijini, na  na kutilia mkazo uimarishaji wa  ushirika ambao  ndiyo soko kubwa kwa mkulima.

 

Kuhusu sekta ya madini ambayo pia ni eneo muhimu la uchumi mkoani Shinyanga, Serikali pia  imeahidi kuendelea  kuhamasisha wachimbaji wakubwa kuja kuwekeza wakati huohuo ikiwahimiza  kutimiza wajibu wao kwa jamii inayowazunguka.

 

Aidha Rais amesema kuwa kazi kubwa inafanyika ya kuwaendeleza wachimbaji wadogo na kuyahimiza makampuni wakubwa kuwaendeleza wachimbaji hao.

 

Akizungumzia tatizo kubwa la maji Mkoani Shinyanga, Rais amesema  kuwa  Serikali imetenga Tshs. Bil. 250 katika bajeti ya maendeleo kwa ajili ya kutatua tatizo la maji Mkoani Shinyanga.

 

Rais amehitimisha ziara yake mkoani  Shinyanga na kurejea Dar es Salaam.

 

Mwisho.