DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

 

Telephone: 255-22-2114512, 2116898

E-mail:  ikulumawasiliano@yahoo.com

               press@ikulu.go.tz             

Fax: 255-22-2113425

 

     PRESIDENT’S OFFICE,

    THE STATE HOUSE,

    P.O. BOX 9120,  

    DAR ES SALAAM.

             Tanzania.

 

 

 

 

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

 

 

Rais Jakaya Mrisho Kikwete leo (Jumatano, Februari 6, 2008) amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Jamhuri ya Saharawi katika Tanzania, Habiballah Abdallahi.

 

Balozi Abdallahi alikuwa anamwaga Rais Kikwete baada ya balozi huyo kuwa amemaliza muda wake wa utumishi wa nchi yake katika Tanzania.

 

Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika Ikulu, Dar Es Salaam, Rais Kikwete alimwakikishia balozi huyo kuwa kamwe Tanzania haiwezi kusahau mapambano ya wananchi wa Saharawi katika kutafuta haki yao ya kuwa huru.

 

Amesema kuwa Tanzania inaelewa fika madai ya haki ya wananchi wa Saharawi kutaka kujitawala.

 

Naye Balozi Abdallahi, mbali na kumpongeza Rais Kikwete kwa kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU) alimwambia pia kuwa binafsi anasikitika kuondoka Tanzania.

 

Balozi Abdallahi alimweleza Rais Kikwete kuhusu mchakato wa mazungumzo kati ya Saharawi na nchi ya Morocco ambayo yanalenga kuondolewa kwa utawala wa Morocco katika nchi hiyo.

 

MWISHO.

 

 

Kurugenzi ya Mawasiliano,

Ikulu.

        06/02/2008