DIRECTORATE
OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
UNITED
|
Telephone: 255-22-2114512, 2116898 E-mail: ikulumawasiliano@yahoo.com Fax: 255-22-2113425
|
|
PRESIDENT’S OFFICE, THE
STATE HOUSE, P.O. BOX 9120, DAR
ES SALAAM. Tanzania. |
TAARIFA
KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais
Jakaya Kikwete amemtumia salamu za pole Mkuu wa Mkoa na wananchi wa Mkoa wa
Manyara kutokana na maafa makubwa yaliyowapata wachimbaji madini katika
machimbo ya Tanzanite ya Mererani, Wilayani Simanjiro, mkoani humo.
Rais
amepokea kwa masikitiko, huzuni na mshtuko mkubwa taarifa ya janga
Rais
Kikwete amehuzunishwa na upotevu wa maisha ya watu ambao mpaka sasa
imethibitika kuwa wamepoteza maisha, yaliyosababishwa na kujaa kwa maji katika
mashimo ya machimbo hayo kutokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha.
Rais
pia anawaombea wachimbaji ambao taarifa zao hazijathibitika waweze kupatikana
haraka wakiwa hai na salama. Rais Kikwete pia anawaombea wote walioumia katika
ajali hiyo kupona haraka.
Rais
anatoa pole kwa familia ambazo zimeathirika na janga
Kurugenzi
ya Mawasiliano ya Rais na Habari,
Butiama,
Mara
Jumapili,
30 Machi 2008.