DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

 

Telephone: 255-22-2114512, 2116898

E-mail:  ikulumawasiliano@yahoo.com

              press@ikulu.go.tz             

Fax: 255-22-2113425

 

 

PRESIDENT’S OFFICE,

      THE STATE HOUSE,

       P.O. BOX 9120,  

DAR ES SALAAM.

Tanzania.

 

 

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

 

SALAMU ZA RAMBIRAMBI ZA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA JAKAYA MRISHO KIKWETE KWA FAMILIA YA MAREHEMU MZEE CHEDIEL MGONJA

 

          Nimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya kifo cha Mzee Chediel Mgonja kilichotokea tarehe 30 Januari, 2009 katika Hospitali ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania ya Lugalo mjini Dar es Salaam.  Wakati huu mkijiandaa kwa mazishi yake, napenda kutumia nafasi hii kutoa mkono wa rambirambi kwenu na kwa ndugu zenu wote.

 

Nilimfahamu Ndugu Mgonja wakati akiwa katika Utumishi wa Umma, akiwa Waziri wa Serikali katika Wizara mbalimbali zikiwamo Wizara ya Mambo ya Nje, na pia Wizara ya Elimu.

 

Alikuwa ni mtumishi hodari, mahiri, mwaminifu na mwadilifu. Amechangia maendeleo ya nchi yetu katika nafasi hizo mbalimbali na tutaendelea kukumbuka mchango wake huo muhimu katika uhai wa taifa letu.

 

            Naungana nanyi katika wakati huu mgumu na wa majonzi makubwa kutokana na msiba mkubwa uliowakuta.  Tunaelewa machungu mliyonayo kutokana na kuondokewa na mpendwa wenu na kiongozi wa familia.  Lakini ni kazi ya Mungu na haina makosa.

 

            Tunawatakia mazishi mema na kuwaombeeni kwa Mungu muwe na nguvu ya kutosha kuweza kuvumilia majonzi ya msiba huu .  Tuzidi kumuombea marehemu, apate mapumziko mema.  Amin.

 

Imetolewa na:

 

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,

Ikulu,

DAR ES SALAAM.

 

31 Januari, 2009