PRESS
SECRETARY TO THE PRESIDENT
Fax. No. 255-22 2113425 The State House,
Tel:
DAR ES SALAAM.
E-mail: press@ikulu.go.tz
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
PREMI KIBANGA,
10.10.2006
Rais Jakaya Mrisho Kikwete leo ametembelea
kituo cha umeme cha masista wa Benedictine walioko Chipole katika wilaya ya
Songea vijijini, mradi ambao unatumika kwa matumizi ya kuendesha shughuli za
kituo cha masista hao zikiwemo shule, nyumba zao za kuishi na kituo cha afya.
“Matatizo
yenu nitayashughulikia kwa vitendo, nitachangia katika shughuli zenu ili
mfanikiwe kwani mkifanikiwa nami nimefanikiwa” Rais amesema wakati wa kujibu
risala ya mama mkuu Maria Shukran
Mkonde, mama mkuu wa kituo cha masista aliyemtaka Rais kuwasaidia kuendeleza
mradi huo wa umeme na kuupanua zaidi kuweza kusaidia hata vijijini vilivyo
jirani.
Kulingana
na taarifa za mradi huo, mradi unaweza kuendelezwa na kutoa huduma kwa maeneo
ya jirani wilayani hapo ambayo kwa sasa hayana huduma za umeme.
Kituo cha
mradi wa umeme cha Masista cha Benedictine kimeanzishwa kwa nguvu za mhisani
kutoka Uswisi mwanzoni mwa mwaka 2000 ambaye ameshafariki dunia kabla ya
kuendeleza mradi huo zaidi ambao una uwezo wa kuzalisha kilowatts 400 kutokana
na maji ya Mto Lupilo.
Jana
(9.10.06) Rais alitembelea kituo cha kuzalisha miche na vikonyo vya kahawa
isiyoshambuliwa na maradhi wala wadudu cha Ugano.
Mara baada
ya kuwasili mkoani hapa, Jumapili tarehe 8.10.06, Rais alipokea taarifa ya mkoa
na chama na baadaye kuzindua jengo la SACCOS , kituo cha Afya cha Mjimwema na
kutembelea makao makuu ya Brigedi ya 401, iliyoko Chandamali ambapo alizungumza
na wapiganaji.
Katika
ziara yake hiyo tangu kuwasili hapa mkoani, Rais pia ametembelea hosteli ya
masista ya Mbamba Bay na kutembelea mradi wa umwagiliaji maji mashamba ya
mpunga yaliyoko Lundo pamoja na kufanya mikutano ya hadhara katika sehemu
mbalimbali ambapo amewashukuru wananchi kwa kumpa kura zilizomwezesha kuwa Rais
wa nchi hii.
‘Serikali
inafanya mageuzi katika kilimo kwani ndiyo shughuli kubwa ya wananchi na ndiyo
inayoweza kuwaondolea umaskini, tunataka kufikia mahali ambapo shughuli zenu
hizi za kilimo zitawaongezea mapato yenu mara mbili ya mnavvopata sasa’ Alisema
Rais.
Pia
amesema katika mageuzi haya ya kilimo serikali itawapa shughuli ya kufanya wale wasio nazo kwa sasa kwa kuongeza matumizi ya maji, yaani kilimo cha
kumwagilia ambapo wananchi watakuwa na uhakika wa kuvuna, kuhamasisha matumizi
ya mbegu bora na za kisasa, na matumizi ya mbolea ambapo mpaka sasa matumizi
yameongezeka mara tatu zaidi ya hapo awali.
Pia
serikali inafanya mpango wa kuweka umeme katika wilaya za mkoa huu pamoja na
kutengeneza barabara kwa kiwango cha lami.
“Tutatengeneza
barabara ya Ruvuma -Mtwara na Mbaba Bay hadi kiwango cha lami na baada ya muda
mfupi tutakuwa na uhakika wa barabara ya Masasi-Tunduru na baadaye
Tunduru-Matemanga-Songea hadi
Rais pia
amewaasa wananchi wa mkoa wa
Kesho Rais
ataelekea Mtwara ambapo pia atafanya ziara ya kutembelea wananchi na kuona
maendeleo
Mwisho