UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

 

Telephone: 255-22-2114512, 2116539

E-mail: press@ikulu.go.tz

Website:  www.mawasilianoikulu.go.tz  

Fax: 255-22-2113425

 

 

PRESIDENT’S OFFICE,

      THE STATE HOUSE,

       P.O. BOX 9120,  

DAR ES SALAAM.

Tanzania.

 

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais Jakaya Mrisho Kikwete leo mchana katika Ikulu ya Dar-Es-Salaam amempokea na kufanya mazungumzo na Rais  wa Muungano wa Visiwa vya Comoro Mheshimiwa Ahmed Abdallah Sambi.

Nimekuja kukushukuru wewe binafsi na Tanzania kwa mchango mkubwa mliotoa kwa nchi yangu ya Comoro, Comoro sasa imekuwa nchi zaidi, yenye amani na inayoendelea, naomba uendelee na moyo huo huoRais Sambi amemwambia Rais Kikwete.

Rais  Sambi pia amemwomba Rais Kikwete aendelee kumsaidia na kumpa ushirikiano zaid Rais mpya aliyechaguliwa tarehe 26 Disemba, 2010, kufuatia uchaguzi mkuu visiwani humo ambao kwa mara ya kwanza,  uchaguzi huo ulihusisha uchaguzi wa Rais wa Muungano wa Visiwa hivyo na pia wa magavana wa Visiwa vya Ngadzija, Anjouan na Moheli.

Rais Kikwete amempongeza Rais Sambi kwa kuongoza uchaguzi huo uliofanyika kwa amani na utulivu na kumhakikishia kuwa Tanzania itaendelea kutoa ushirikiano kwa uongozi wa visiwa hivyo. Katika uchaguzi huo wa Disemba 26, 2010 Dkt. Ikililou Dhoinine aliibuka mshindi.

Wakati huo huo Rais Kikwete ameelekea Mkoani Iringa jioni hii kwa ajili ya kushiriki maziko ya mama Mzazi wa Mheshimiwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Bibi Tulakela Milia Samnyuha  yatakayofanyika kijijini kwao  Yakobi  wilayani  Njombe kesho Mei 8, 2011.

Mara baada ya kupata taarifa za kifo cha mama mzazi wa Spika, kilichotokea tarehe 5 Mei, 2011,  Rais Kikwete alimtumia salamu za pole Mhe. Spika kwa niaba yake, familia yake na Watanzania kwa ujumla na kumuombea mapumziko mema marehemu Bibi Samnyuha.

Mara baada ya maziko hayo Rais Kikwete ataelekea Dodoma kwa ajili ya kuhudhuria Semina Elekezi  kwa ajili ya Mawaziri na Viongozi Waandamizi wa Serikali itakayoanzaJumatatu tarehe 9 Mei, 2011.

Mwisho

 

Imetolewa na Premi Kibanga,

Mwandishi wa Habari wa Rais Msaidizi,

Ikulu.

Dar es Salaam.

7 Mei, 2011