UNITED
DIRECTORATE
OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
|
Telephone: 255-22-2114512, 2116898 E-mail: press@ikulu.go.tz Fax: 255-22-2113425
|
|
PRESIDENT’S OFFICE, THE STATE HOUSE, P.O. BOX 9120,
DAR ES SALAAM. Tanzania. |
TAARIFA KWA VYOMBO
VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Dkt.
Servacius Beda Likwelile kuwa Naibu Katibu Mkuu katika Wizara ya Fedha na
Uchumi, taarifa iliyotolea Ikulu, Dar es Salaam, leo, Alhamisi, Mei 20, 2010,
imeeleza.
Taarifa hiyo iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi, Bwana Phillemon L. Luhanjo imesema
kuwa uteuzi huo ulianza Mei 10, mwaka huu, 2010.
Kabla ya uteuzi wake, Dkt. Likwelile alikuwa
Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii
(TASAF).
Dkt. Likwelile anachukua nafasi
iliyoachwa wazi na Dkt. Philip Mpango aliyeteuliwa
karibuni kuwa Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango.
Imetolewa
na:
Kurugenzi
ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR
ES SALAAM.
20
Mei, 2010