DIRECTORATE
OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
UNITED
|
Telephone: 255-22-2114512, 2116898 E-mail: ikulumawasiliano@yahoo.com Fax: 255-22-2113425
|
|
PRESIDENT’S OFFICE, THE STATE HOUSE, P.O. BOX 9120,
DAR ES SALAAM. Tanzania. |
TAARIFA KWA
VYOMBO VYA HABARI
SALAMU ZA
RAMBIRAMBI ZA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA
MRISHO KIKWETE
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amemtumia salamu za rambirambi
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa Mkoa wa Mbeya, Bwana Nawab Mullah
kutokana na kifo cha Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya ya Kyela, Marehemu Japhet
Mwakasumi, aliyefariki tarehe 19 Mei, 2010 Jijini Dar es Salaam.
Katika salamu zake hizo, Rais Jakaya
Kikwete amesema amesikitishwa na kuhuzunishwa
“Ninatambua vema mchango wa Marehemu
Mwakasumi wakati wa uhai wake katika Wilaya ya Kyela hususan katika Chama Cha
Mapinduzi kutokana na uhodari na uchapakazi wake ambao umeiwezesha CCM
kuimarika zaidi, “amesema Rais Kikwete na kuongeza, “Kwa hakika kifo chake ni
pigo kubwa kwa familia yake, wana – CCM na wananchi wote wa Wilaya ya Kyela,
Mkoa wa Mbeya na Taifa kwa ujumla”.
Katika rambirambi zake kwa familia ya
Marehemu Japhet Mwakasumi, Rais Kikwete amesema familia hiyo imepoteza kiongozi
muhimu. Amewataka ndugu, jamaa na
marafiki wa Marehemu Mwakasumi kuwa na moyo wa uvumilivu na subira katika
kipindi hiki kigumu cha maombolezo, na amemuomba Mwenyezi Mungu ailaze mahali
pema peponi roho ya Marehemu Japhet Mwakasumi.
Imetolewa
na:
Kurugenzi
ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
21
Mei, 2010