UNITED REPUBLIC OF
TANZANIA
DIRECTORATE OF
PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
|
Telephone: 255-22-2114512, 2116539 E-mail: press@ikulu.go.tz Website: www.mawasilianoikulu.go.tz Fax: 255-22-2113425
|
|
PRESIDENT’S
OFFICE, THE STATE HOUSE, P.O. BOX
9120, DAR ES SALAAM. Tanzania. |
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuriya
Muunganowa Tanzania, Mheshimiwa
Jakaya Mrisho Kikwete amesema kuwa misaada ya
Marekani kwa Tanzania inachangia kwa kiasi kikubwa kujenga
Tanzania ijayo na kuokoa maisha ya
maelfu kwa maelfu ya Watanzania.
Aidha, Rais Kikwete amesema
kuwa misaada hiyo ya Marekani
kwa Tanzania inasaidia kupunguza shinikizo kwenye bajeti ya Serikali
ambayo katika hali ya kawaida
ingetumia fedha yake katika kutoa
huduma kwenye maeneo yanayo saidiwa
na Marekani.
Rais Kikwete ameyasema hayo leo,
Alhamisi, Mei 5, 2011, wakati
alipokutana na kufanya mazungumzo na Naibu Waziri
wa Mambo ya Nje ya Marekani
anayeshughulikia Menejimenti
na Raslimali, Bwana Thomas Nides na ujumbe
wake.
Rais Kikwete yuko Afrika
Kusini kuhudhuria Mkutano wa
21 wa Uchumi Duniani wa World Economic Forum –
Africa wakati Bwana Nides yuko katika ziara
ya nchi za
Afrika na amewasili mjini Cape Town akitokea Mozambique.
Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika kwenye Hoteli ya One & Only mjini Cape Town ambako Rais Kikwete amefikia,
Rais Kikwete amemshukuru Naibu Waziri huyo akisema:
“Misaada ya Marekani imesaidia
sana kuokoa
maisha ya maelfu kwa maelfu
ya wananchi wetu na pia
kutoa huduma muhimu kwa wananchi
na kuchangia uchumi wetu. Tunawashukuru
sana kwa
sababu mnasaidia kujenga misingi imara ya maendeleo
imara ya nchi yetu.”
Marekani imekuwa mmoja wa wabia wakubwa wa maendeleo
ya Tanzania ikisaidia katika sekta muhimu
kama vile elimu, afya na miundombinu.
Katika eneo la elimu, kwa mfano,
Marekani inasaidia kugarimia uchapaji wa vitabu vya
sayansi kwa ajili ya shule
za sekondari nchini.
Katika eneo la afya, Marekani
kupitia Mpango Maalum wa Afya
wa Rais wa
Marekani uitwao PEPFAR, imechangia sana katika kupambana na magonjwa ya
malaria na Ukimwi ikiwa ni pamoja
na kutoa dawa za kusaidia
kurefusha maisha ya watu wanaoishi
na virusi vya ukimwi. Katika eneo la miundombinu, Marekani kupitia mpango wake wa
MCC inasaidia ujenzi wa barabara muhimu
nchini, na miradi mingine muhimu kama vile ya umeme, ujenzi
wa viwanja vya ndege, na
miradi ya maji ambayo yote
imeanza kutekelezwa.
“Katika eneo la malaria na
ukimwi, kwa mfano, Marekani imechangia mno kuokoa maisha ya
wananchi wetu. Kule Tanzania Visiwani, malaria sasa imeanza kuwa
historia na
kwa upande wa Tanzania tumepunguza malaria kwa asilimia 40,” amesema Rais Kikwete
na kuongeza:
“Katika ukimwi, maelfu kwa maelfu ya
watu wetu wanapata dawa za
kurefusha maisha na kiasi cha Watanzania milioni 13 wamekwisha kupima ukimwi katika
mpango unaosaidiwa na Marekani.”
Rais Kikwete pia amekutana
na kufanya
mazungumzo na Makamu wa Rais
na Meneja Mkuu wa Dunia
wa Kampuni ya Intel, Bwana John Davies.
Jana usiku, Rais Kikwete pia
alikutana na
kufanya mazungumzo na Naibu Mwenyekiti
wa Tume ya
Umoja wa Afrika, Erasto Mwencha na pia
alikutana na Mtendaji Mkuu wa
NEPAD Ibrahim Mayaki.
Imetolewa na:
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais,
Safarini,
Cape
Town, Afrika Kusini
5
Mei, 2011