UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

 

Telephone: 255-22-2114512, 2116539

E-mail: press@ikulu.go.tz

Website:  www.mawasilianoikulu.go.tz  

Fax: 255-22-2113425

 

Coat of Arms

 

PRESIDENT’S OFFICE,

      THE STATE HOUSE,

       P.O. BOX 9120,  

DAR ES SALAAM.

Tanzania.

 

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

 

Na MwandishiMaalum, Cape Town, AfrikaKusini

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amesema kuwa uongozi wake hauna muda tena wa kupoteza katika kuhakikisha kuwa wakulima wa Tanzania wanainuliwa kutoka kwenye umasikini kwa kuhakikisha kuwa kilimo cha Tanzania kinaboreshwa haraka iwezekanavyo.

 

Wangu ni uongozi usiokuwa na muda wa kupoteza. Nina haraka. Sina muda tena wakusubiri. Tunahitaji kuongeza kasi ya mapambano ya kuwatoa wakulima wetu katika umasikini. Watu wetu wameishi katika umasikini kwa miaka mingi kupita kiasi. Watu wetu wameteseka sana,” Rais Kikwete amesema leo, Jumatano, Mei 4, 2011.

 

Rais Kikwete ameyasema hayo wakati anashiriki katika kikao maalum cha kujadili jinsi ya kuanzisha Soko la Mazaola Tanzania (Tanzania Commodity Exchange) ikiwani sehemu ya Mkutano wa 21 wa Mkutano wa Uchumi Duniani, Kanda ya Afrika, unaofanyika kwenye Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Mjini Cape Town, AfrikaKusini.

 

Mkutano huo ambao mwaka jana ulifanyika mjini Dar es Salaam, ikiwa ni mara ya kwanza kufanyika nje ya Jiji la Cape Town, umeanza leo mchana na mada kuu ya mkutano wa mwaka huu ni Nafasi ya Afrika katika Mazingira Halisi Mapya Duniani (Africa’s Role in the New Reality).

Akifunga kikao hicho kuhusu uanzishwaji wa Soko la Mazao katika Tanzania, Rais Kikwete amewaambia washiriki kuwa wakati umefika wa kukabiliana na umasikini ana kwa ana kwa nia ya kuupunguza na hatimaye kuumaliza kabisa kwasababu wananchi wameishi katika maisha ya shida na dhiki kwa miaka mingi sana.

 

Washiriki wa kikao hicho walijadili uanzishwaji wa Soko hilo baada ya mawasilisho yaliyofanywa na mtaalamu wa masoko ya mazao, Bwana Barat.  Katika mawasilisho yake, Bwana Barat ameeleza jinsi soko la mazao la Ethiopia alilosaidia kuanzisha katika miaka ya karibuni linavyoshamiri.

         

Bwana Barat pia ametoa maelezo ya jumla ya jinsi soko la mazao linavyotakiwa kufanya kazi, nani analimiki, nani analidhamini, nani anatoa fedha za uanzishwaji wake, nani wanashiriki katika shughuli zake, nani ananufaika nalo na kwa kiasi gani.

 

Aidha, Bwana Barat ameeleza muundo anaoupendekeza kwa ajili ya Soko la Mazao la Tanzania ambalo anapendekeza kuwa lianzeshughuli zake kabla ya mwisho wa mwaka huu.

 

Bwana Barat amesema kuwa moja ya malengo makuu ya soko hilo litakuwa ni kuwageuza wakulima wa Tanzania kutoka katika kilimo cha kujikimu na kuwafanya wajasiria mali katika kilimo ili waweze kunufaika kwa kiasi kinachostahili na jasho lao.

         

          Mwisho.

 

Imetolewa na:

 

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais,

Safarini,

Cape Town, Afrika Kusini

 

05 Mei, 2011