DIRECTORATE
OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
UNITED
|
Telephone: 255-22-2114512, 2116898 E-mail: ikulumawasiliano@yahoo.com Fax: 255-22-2113425
|
|
PRESIDENT’S OFFICE, THE STATE HOUSE, P.O. BOX 9120,
DAR ES SALAAM. Tanzania. |
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
SALAMU ZA RAMBIRAMBI ZA RAIS WA
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA JAKAYA MRISHO KIKWETE
Rais
wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania, Mheshimwia Dkt. Jakaya Mrisho
Kikwete amemtumia salamu za rambirambi
Mkuu wa Mkoa
wa Mwanza, Mheshimiwa Abbas Kandoro kufuatia vifo vya watu
16 vilivyotokea tarehe 17
Mei, 2011 baada ya mabasi mawili kugongana
uso kwa uso
mkoani Mwanza.
Ajali hiyo iliyotokea katika Kijiji cha Chibingo wilayani Geita ilihusisha mabasi makubwa mawili ya abiria;
basi la Bunda Express lililokuwa likitokea Mwanza kwenda Karagwe
mkoani Kagera ambalo liligongana uso kwa uso na basi
lingine la Sheraton lililokuwa
likitokea Bukombe Mkoani Shinyanga likielekea Mwanza.
“Kufuatia ajali hiyo, ninakutumia
salamu za rambirambi wewe Mkuu wa Mkoa, Mheshimiwa Abbas Kandoro kutokana
na msiba huo mkubwa. Pia kupitia kwako, natuma salamu za
rambirambi kwa familia na watu
wote waliopoteza ndugu zao katika
ajali hiyo mbaya”, amesema kwa masikitiko
Rais Kikwete katika salamu zake
hizo, na kuongeza,
“Ninamuomba
Mwenyezi Mungu mwingi wa
Rehema azipokee na kuziweka mahali
pema peponi roho za marehemu
wote.”
Aidha Rais Kikwete amewahakikishia
wafiwa wote kuwa yupo pamoja
nao katika kuomboleza vifo vya wapendwa wao
huku akiwaomba wawe na moyo wa uvumilivu,
ujasiri na subira katika kipindi
hiki kigumu cha maombolezo.
Kwa upande mwingine Rais Kikwete anawaombea
kwa Mola
wote waliojeruhiwa katika ajali hiyo
waweze kupona haraka na kurejea
katika hali zao za kawaida ili hatimaye waungane
tena na familia,
ndugu, jamaa na marafiki zao.
Rais kikwete amezitaka mamlaka na
vyombo vyote vinavyohusika na usimamizi wa Sheria
ya Usalama Barabarani kutekeleza kikamilifu wajibu wao, kwani, amesema
kuwajibika kwao kuna mchango mkubwa
katika kudhibiti na hata kutokomeza
kabisa ajali za barabarani zinazotokana
na uzembe wa baadhi ya
madereva hususan wa mabasi ya
abiria wasioheshimu Sheria ya Usalama
Barabarani.
Imetolewa
na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
18
Mei, 2011