DIRECTORATE
OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
UNITED
|
Telephone: 255-22-2114512, 2116898 E-mail: press@ikulu.go.tz Fax: 255-22-2113425
|
|
PRESIDENT’S OFFICE, THE
STATE HOUSE, P.O. BOX 9120, DAR
ES SALAAM. Tanzania. |
04 Machi, 2009
Mkurugenzi Mtendaji,
Kituo cha Televisheni,
ITV/Radio One,
S.L.P. 4374,
DAR ES SALAAM.
Ninakujulisha kuwa
nimesikitishwa na
kuhuzunishwa sana na taarifa za
kifo cha mtangazaji wa Kituo cha Televisheni
cha ITV, Rehema Mwakangale kilichotokea siku ya Jumanne tarehe
03 Machi, 2009 katika Hospitali ya Mission Mikocheni Jijini Dar es Salaam alikokuwa amelazwa akisumbuliwa na maradhi ya
kifua.
Binafsi nilimfahamu
marehemu Mwakangale kutokana na
uchapakazi wake na umakini katika fani ya utangazaji
ambayo ilimwezesha kuwafikishia wananchi habari mbalimbali za kiuchumi na
kijamii kupitia Kituo cha Televisheni cha
ITV. Kifo chake ni
pigo kubwa kwa Watanzania wote na hasa
wanataaluma wenyewe wa Uandishi wa
Habari hapa nchini.
Kutokana na msiba huo mkubwa, ninakutumia
salamu zangu za rambirambi kwa
kumpoteza mmojawapo wa wafanyakazi muhimu katika kituo
chako. Aidha, kupitia kwako, natuma salamu
za rambirambi kwa familia,
ndugu, jamaa na marafiki wa
marehemu Rehema Mwakangale. Nawaombeni nyote muwe na moyo wa ujasiri
na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo.
Mwenyezi Mungu ailaze roho
ya marehemu Rehema Mwakangale mahali pema peponi.
Jakaya Mrisho
Kikwete
RAIS
WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA