UNITED REPUBLIC OF
TANZANIA
DIRECTORATE OF
PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
|
Telephone: 255-22-2114512, 2116539 E-mail: press@ikulu.go.tz Website: www.mawasilianoikulu.go.tz Fax: 255-22-2113425
|
|
PRESIDENT’S
OFFICE, THE STATE HOUSE, P.O. BOX
9120, DAR ES SALAAM. Tanzania. |
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Chama cha Wanasheria
cha Afrika Mashariki (EALS)
kimempongeza Rais wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete
na Serikali yake kwa kuanzisha
na kuruhusu mjadala wa sasa
wa nchi nzima
kuhusu mabadiliko ya Katiba katika
Tanzania.
Aidha, chama hicho kimeipongeza
Tanzania kwa kuwa nchi pekee katika
Afrika na ya nne katika
Bara la Afrika kwa kupitisha utekelezaji na kuruhusu watu
binafsi uhuru wa kuutumia Mkataba
wa Afrika na Wananchi wa
Afrika wa Haki za Binadamu.
Pongezi hizi zimetolewa leo, Jumanne, Aprili
5, 2011, na viongozi wa chama hicho
wakiongozwa na Rais wa EALS, Dk. Wilbert B Kapinga wakati viongozi hao walipokutana
na kufanya mazungumzo na Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, Mheshimiwa Jakaya
Mrisho Kikwete, Ikulu, Dar es Salaam.
Viongozi hao wa kamati mpya ya
uongozi ya EALS iliyochaguliwa Novemba 19, mwaka jana, katika
Mkutano Mkuu wa chama hicho
uliofanyika Bujumbura, Burundi, wanatoka
katika nchi zote wanachama wa Jumuia ya
Afrika Mashariki za Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda na
Burundi. Pia uongozi huo unashirikisha viongozi kutoka Tanzania Visiwani.
Katika taarifa yake iliyosomwa
mbele ya Mheshimiwa Rais Kikwete na
Dk. Kapinga, EALS imesema:
“Tunapenda kuupongeza sana uongozi wako
na Serikali yako kwa kuruhusu
mjadala mpana wa sasa kuhusu
mabadiliko ya Katiba ya Tanzania.”
Katika
taarifa hiyo, viongozi hao pia
wamwomba Rais Kikwete kuwasaidia kupata kiwanja vya kujenga makazi
ya kudumu ya chama hicho
mjini Arusha yalipo makao makuu
cha chama hicho.
Aidha, viongozi hao wamemwomba
Rais Kikwete kuangalia jinsi ya kusaidia kukiwezesha
chama hicho kuweza kuingiza nchini kwa urahisi
zaidi maofisa wake kutoka nchi jingine
wanachama wa EALS wanaopata
kazi kwenye makao makuu mjini
Arusha.
Rais
Kikwete ameahidi kuwa atayafuatilia mambo hayo mawili kuona
jinsi gani chama hicho kinavyoweza
kusaidiwa bila kukwazika kupita kiasi.
Wakati huo huo, Rais
Kikwete amepokea ujumbe maalum kutoka
kwa Rais
Paul Kagame wa Rwanda. Ujumbe huo umewasilishwa
na Waziri
wa Sheria na Mwanasheria Mkuu wa Rwanda, Mheshimiwa Tharcisse Karugarama ambaye pia ni mjumbe
maalum wa Rais Kagame.
Mheshimiwa Karugarama ameandamana na Balozi
wa Rwanda katika Tanzania, Mheshimiwa Fatuma Ndangiza.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano
ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
04
Aprili, 2011