DIRECTORATE
OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
UNITED
|
Telephone: 255-22-2114512, 2116898 E-mail: press@ikulu.go.tz Fax: 255-22-2113425
|
|
PRESIDENT’S OFFICE, THE
STATE HOUSE, P.O. BOX 9120, DAR
ES SALAAM. Tanzania. |
TAARIFA
KWA VYOMBO VYA HABARI
Na Mwandishi Maalum
Rais Jakaya Mrisho Kikwete ameliambia Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa
(UNDP) kuwa hali ya ukame katika
baadhi ya sehemu za
Amelitaka Shirika
Aidha, Rais Kikwete amesifia mfumo mpya wa Umoja wa Mataifa wa
Delivering as One ambako
shughuli za Umoja huo zinafanyika
kwa pamoja baina ya mashirika
mbalimbali ya Umoja huo na
kusema kuwa mfumo huo una
manufaa kwa UN yenyewe na nchi
wanachama wa Umoja huo.
Akizungumza leo, Jumanne, Novemba 3, 2009, na Bwana Alberic Kacom, Mratibu wa Shughuli
za Umoja wa Mataifa mpya
katika
“Mwaka huu, kuna
dalili kuwa hatutapa mvua za
kutosha katika baadhi ya sehemu
za nchi yetu. Kwa kawaida mvua huanza
Oktoba na
wakati huu nchi inakuwa imelowa
maji. Na kwa
kweli tukikosa mvua za vuli,
hali itakuwa mbaya,” amesema Rais.
Ameongeza: “Kwa miaka miwili iliyopita,
tumekuwa na
matatizo ya mvua na katika
baadhi ya maeneo ya nchi
yetu ukame unazidi kuwa mkali
zaidi.”
“Hali hii inatia wasiwasi
Kuhusu mfumo mpya wa
UN, Rais amesema kuwa mfumo huo
wa Delivering
as One umethibitika kuwa
ni mfumo mzuri na unaofaa
kuanza kutumiwa katika nchi zote
duniani. Mfumo huo umekuwa ukifanyiwa majaribio katika nchi nane
duniani, ikiwamo
Kuhusu matatizo ya sasa ya
mgao wa
umeme, Rais Kikwete amesema kuwa matatizo ya
sasa ya umeme
ni ya muda
tu na kuwa
Serikali yake inachukua kila hatua kuyamaliza.
Amesema kuwa kwa hakika,
upo umeme wa kutosha kuondokana
na mgao wa
sasa na ndio
maana amechukua hatua za kuhakikisha
kuwa mitambo ya kampuni ya
Independent Power Tanzania Limited (IPTL) inawashwa, ili kuziba pengo
la sasa katika Gridi ya Taifa.
Imetolewa na:
Kurugenzi
ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
03
Novemba, 2009