UNITED REPUBLIC OF
TANZANIA
DIRECTORATE OF
PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
|
Telephone: 255-22-2114512, 2116539 E-mail: press@ikulu.go.tz Website: www.mawasilianoikulu.go.tz Fax: 255-22-2113425
|
|
PRESIDENT’S
OFFICE, THE STATE HOUSE, P.O. BOX
9120, DAR ES SALAAM. Tanzania. |
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo, Ijumaa, Machi
25, 2011, ametia saini kitabu cha maombolezo kufuatia upotevu wa maisha ya
maelfu kwa maelfu ya wananchi
wa Japan ambao wamepoteza maisha yao katika tsunami na tetemeko kubwa
la ardhi lililotokea Machi 11, mwaka huu, nchini humo.
Rais Kikwete ametia saini kitabu hicho
jioni ya leo kwenye
Ubalozi wa Japan ulioko Upanga, mjini Dar es Salaam. Pamoja naye alikuwa Waziri
wa Mambo ya
Nje na Ushirikiano
wa Kimataifa Mheshimiwa Bernard Membe ambaye naye ametia
saini kitabu hicho.
Kwenye ubalozi huo, Rais
Kikwete amepokelewa na Balozi
wa Japan katika Tanzania Mheshimiwa Hiroshi Nakagawa na maofisa wengine wa ubalozi huo.
Akizungumza
kwa ufupi tu baada ya
kuwa ametia saini kitabu hicho,
Rais Kikwete ametoa salamu za
rambirambi kwa nchi hiyo ya
Japan ambayo ameielezea kama rafiki wa
siku nyingi kwa upotevu mkubwa
wa maisha na mali kutokana
na tsunami iliyoambatana na tetemeko kubwa
la ardhi.
Mara
tu baada ya tukio hilo la huzuni kubwa, Serikali ya Tanzania ilituma salamu rasmi za
rambirambi kwa Serikali ya Japan.
Mwisho.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR
ES SALAAM.
25 Machi, 2011