UNITED
DIRECTORATE
OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
|
Telephone: 255-22-2114512, 2116898 E-mail: ikulumawasiliano@yahoo.com Fax: 255-22-2113425
|
|
PRESIDENT’S OFFICE, THE STATE HOUSE, P.O. BOX 9120,
DAR ES SALAAM. Tanzania. |
TAARIFA KWA
VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, usiku wa jana,
Jumatatu, Septemba 5, 2011,
amekutana na kufanya mazungumzo na Masheikh wa
Dini ya Kiislam
kuhusu mchakato wa kuundwa kwa
Mahakama ya Kadhi nchini.
Katika mkutano huo, pande
hizo mbili zimezungumzia kwa
undani hali ya majadiliano ya suala zima
la kuanzishwa kwa Mahakama hiyo ya
Kadhi.
Mheshimiwa Rais na Masheikh wamekubaliana kuwa Kamati ya
Pamoja ya Serikali na Masheikh
ikutane mapema iwezekanavyo na iongeze kasi ya
majadiliano ili shughuli hiyo iweze
kumalizika mapema iwezekanavyo.
(Habari hii imeambatana na picha
ya Mheshimiwa Rais na Masheikh
katika kikao hicho cha jana).
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR
ES SALAAM.
06
Septemba, 2011