DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

 

Telephone: 255-22-2114512, 2116898

E-mail: press@ikulu.go.tz             

Fax: 255-22-2113425

 

 

PRESIDENT’S OFFICE,

      THE STATE HOUSE,

       P.O. BOX 9120,  

DAR ES SALAAM.

Tanzania.

 

 

 

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

 

 

Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, jana, Jumanne, Aprili 28, 2010, alishiriki katika mazishi ya watoto wadogo watatu wa shule katika kijiji cha kwao cha Msoga, Chalinze, Wilaya ya Bagamoyo, Mkoa wa Pwani.

 

Watoto hao watatuOmari Mrisho mwenye umri wa miaka 13, Evarist  Semeni mwenye umri wa miaka 11 na Ezekiel George Setumbi, mwenye umri wa miaka 13, walipoteza maisha baada ya kuwa wamegongwa na gari katika ajali iliyotokea usiku wa kuamkia jana hiyo hiyo katika kijiji hicho cha Msoga.

 

Mrisho alikuwa mwanafunzi wa darasa la sita katika Shule ya Msingi ya Msoga, Semeni alikuwa mwanafunzi wa darasa la nne katika Shule ya Msingi ya Msoga vilevile wakati Setumbi alikuwa mwanafunzi wa darasa la sita katika Shule ya Msingi ya Mboga.

 

Imetolewa na:

 

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,

Ikulu,

DAR ES SALAAM.

 

28 Aprili, 2010