DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

Telephone: 255-22-2114512, 2116898

E-mail:  ikulumawasiliano@yahoo.com

              press@ikulu.go.tz             

Fax: 255-22-2113425

 

Coat of Arms

PRESIDENT’S OFFICE,

      THE STATE HOUSE,

              P.O. BOX 9120,  

DAR ES SALAAM.

Tanzania.

 

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Mwaka 2011 umeelezewa kuwa Mwanzo wa Muongo wa Vita Dhidi ya Malaria Barani Afrika. Rais Jakaya Mrisho Kikwete, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Mshikamano wa Viongozi wa Afrika Dhidi ya Malaria (African Leaders Malaria Alliance-ALMA), amesema leo mchana wakati akifungua Kikao cha Viongozi wa Nchi 35 za Afrika zinazounda Mshikamano wa Kupambana na Malaria Barani Afrika.  Mwaka wa 2011 ni Mwanzo wa Muongo Mpya katika Afrika Dhidi ya Malaria, pia unaashiria mstari wa mwisho katika kukaribia mwisho wa juhudi hizi katika kufuta vifo vinavyotokana na malaria kuelekea mwaka 2015”.

Rais Kikwete amesema na kuelezea umuhimu wa hatua hii iliyopigwa na nchi za Afrika katika kufikia malengo ya milenia ambayo yamewekwa na nchi hizi kama wanachama wa familia ya Umoja wa Mataifa.  Kulingana na ripoti ya Shirika la Afya Duniani(WHO) ya mwaka 2010, vifo vinavyotokana na malaria vimepungua Barani Afrika na hii ni kwa sababu ya juhudi za makusudi za kutokomeza malaria, juhudi hizi zimetekelezwa katika nchi mbalimbali kwa kushirikiana na wenza kimataifa.

Katika kikao cha leo nchi nne zimefuzu na kupokea Tuzo ya Kwanza ya Ubora na Umakini katika Juhudi za Kupambana na Malaria zikiwemo Tanzania, Guinea, Kenya na Uganda.  Juhudi zilizofanywa na nchi hizi ni pamoja na kukuza uhusiano na kuharakisha upatikanaji wa fedha, kudhibiti na kukuza matumizi ya kinga ya malaria, mfano ikiwemo matumizi ya vyandarua, kufuta na kusitisha utengenezaji, usambazaji na matumizi ya dawa aina ya Artemisinin, kuondosha kodi na kuunga mkono utengenezaji na uzalishaji wa dawa za malaria Barani Afrika.  Rais Kikwete amepokea tuzo hiyo katika kikao cha leo na kushuhudiwa na nchi wanachama wakiwemo pia Katibu Mkuu wa Umoja wa Mmataifa Ban Ki Moon, mwenyeji wa Mkutano wa Viongozi wa Afrika wanaohudhuria kikao jijini Addis Ababa Waziri Mkuu Meles Zenawi viongozi wa mashirika ya kimataifa na nchi rafiki.

Katika kikao cha leo Rais wa Liberia Ellen Johnson Sirleaf amechaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa ALMA.  Rais Kikwete yuko Addis Ababa kuhudhuria kikao cha Viongozi wa Afrika kinachotazamiwa kumalizika leo jioni.  Rais anatarajiwa kurejea nyumbani kesho tarehe 1 Februari, 2011.

Mwisho.

Imetolewa na Primi Kibanga,

ADDIS ABABA.

Ethiopia.

31 Januari, 2011