UNITED
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
|
Telephone: 255-22-2114512, 2116539 E-mail: press@ikulu.go.tz Website: www.mawasilianoikulu.go.tz Fax: 255-22-2113425
|
|
PRESIDENT’S OFFICE, THE STATE HOUSE, P.O. BOX 9120, DAR ES SALAAM. Tanzania. |
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Msimamo wa
Tanzania juu ya Ivory Coast ni wazi, Rais Kikwete amemwambia Ban Ki Moom
RAIS
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, jana,
Jumatano, Januari 26, 2011, amekutana na kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa
Umoja wa Mataifa, Mheshimiwa Ban Ki Moon.
Aidha,
Rais Kikwete amekutana na kufanya mazungumzo na Mkuu wa Shirika la Maendeleo la
Marekani (USAID), Mheshimiwa Dkt. Rajiv Shah kwenye Hoteli ya Intercontinental
mjini Geneva, Uswisi, ambako Rais Kikwete amefikia.
Rais
Kikwete yuko mjini Geneva kuhudhuria na kuendesha Mkutano wa Kwanza wa Tume ya
Kimataifa Kuhusu Afya ya Akinamama na Watoto ambako yeye ni mwenyekiti mwenza
na Waziri Mkuu wa Canada, Mheshimiwa Stephen Harper. Mkutano huo wa siku moja,
umefanyika mjini Geneva jana vile vile.
Mheshimiwa Ban Ki Moon alikuwa mjini
Geneva kwa ajili ya ufunguzi wa Mkutano wa Tume hiyo inayoongozwa kwa pamoja na
Rais Kikwete na Waziri Mkuu Harper wakati Dkt. Shah ni kamishna katika Tume
hiyo yenye makamishna 30.
Katika
mkutano wake na Mheshimiwa Ban Ki Moon, viongozi hao wawili wamejadili masuala
mbali mbali kuhusu jinsi ya kufanikisha mchakato wa Tume ya Kimataifa Kuhusu
Afya ya Akinamama na Watoto, ambayo imechanguliwa na Umoja wa mataifa kupitia
Shirika la Afya Duniani (WHO).
Mheshimiwa
Ban Ki Moon amemshukuru na kumsifia Rais Kikwete kwa uongozi wake katika suala
zima la afya ya akinamama na watoto na kumweleza kuwa anayo matumaini makubwa
kwake kuwa atafanikisha malengo ya Tume hiyo.
Viongozi
hao wawili pia wamejadili hali ya kisiasa katika Ivory Coast ambako Rais
anayekubaliwa kimataifa kuwa alishindwa uchaguzi mkuu wa Novemba mwaka jana katika
nchi hiyo Bwana Laurent Gbagbo amekataa kukabidhi madaraka ya kuongoza nchi
hiyo kwa Mheshimiwa Alassane Quattara ambaye anakubaliwa kimataifa kuwa
alishinda uchaguzi huo kwa asilimia tisa.
Mheshimiwa
Ban Ki Moon ametaka Umoja wa Afrika (AU), Umoja wa Mataifa (UN) na Umoja wa
Kiuchumi wa Nchi za Afrika Magharibi (ECOWAS) kushirikiana katika kuhakikisha
kuwa demokrasia inadumishwa katika Ivory Coast.
Mheshimiwa
Kikwete amemwambia Katibu Mkuu huyo wa UN kuwa msimamo wa Tanzania ni wazi
kabisa kwamba haikubali mgombea ambaye kila ushahidi unaonyesha kuwa alishindwa
uchaguzi kuendelea kushikilia madaraka.
Naye
Mheshimiwa Ban Ki Moon alisema kuwa vitendo na maamuzi ya Bwana Gbagbo tokea
kushindwa uchaguzi wa nchi hiyo vinahujumu mamlaka, madaka na nafasi ya Umoja
wa Mataifa katika kulinda na kutetea demokrasia na haki duniani.
“Inawezekana
vipi, ushindi wa asilimia tisa wa Quattara ukabadilishwa na kuwa ushindi wa
asilimia moja wa Gbagbo?” ameuliza Mheshimiwa Ban Ki Moon katika
mazungumzo hayo.
Katika
mazungumzo yake na Dkt. Shah, viongozi hao wawili wamejadili jinsi Marekani
ilivyo tayari kuisaidia Tanzania katika kuhakikisha kuwa inajitegemea katika usalama
na uzalishaji wa chakula na pia kuhakikisha kuwa nchi hiyo inapiga maendeleo ya
haraka zaidi kuelekea katika kuwa nchi yenye uchumi na kipato cha kati kwa
wananchi wake.
Dkt.
Shah amemweleza jinsi gani Rais wa Marekani Mhesimiwa Barack Obama amedhamiria
kuendeleza kilimo katika baadhi ya nchi zinazoendelea duniani kama njia ya
kujenga urafiki na ushirikiano wa muda mrefu kati ya Marekani na nchi hizo.
Dkt.
Shah pia ameonya kuwa uchunguzi na habari za uhakika ambazo USAID inazo ni
kwamba bei za chakula na mazao mengine ya kilimo duniani inaweza kuongezeka
tena katika miezi sita ijayo.
Rais
Kikwete na Dkt. Shah pia wamejadili jinsi Marekani itakavyosaidia katika kuunga
mkono jitihada za kuinua kilimo katika mipango ya SAGCOT na Feed the Future.
Mwisho.
Imetolewa na:
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais,
Safarini,
GENEVA.
26 Januari, 2011