UNITED
DIRECTORATE
OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
|
Telephone:255-22-2114512, 2116898 E-mail: ikulumawasiliano@yahoo.com Fax: 255-22-2113425
|
|
PRESIDENT’S OFFICE, THE STATE HOUSE, P.O. BOX 9120, DAR ES SALAAM. Tanzania. |
TAARIFA KWA VYOMBO
VYA HABARI
Rais wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete
leo, Jumanne, Novemba 29, 2011, ametia saini Muswada wa
Sheria ya Mabadiliko ya Katiba
ya Mwaka 2011.
Hatua hiyo ya Mheshimiwa
Rais kutia saini Muswada huo
inakamilisha safari ya kutungwa kwa
Sheria ya Mabadiliko ya Katiba
ya Mwaka 2011 baada ya Bunge kuwa limepitisha Muswada huo uliowasilishwa
na Serikali katika kikao kilichopita
cha Bunge.
Aidha, kutiwa saini kwa
Muswada huo ili uwe Sheria
ni hatua kubwa na muhimu
katika safari ya kutungwa kwa Katiba
mpya ya Tanzania kama ilivyoahidiwa na Mheshimiwa Rais
Kikwete katika salamu zake za
Mwaka Mpya kwa wananchi Desemba
31, mwaka jana, 2010.
Pamoja na kutiwa
saini hiyo bado Serikali itaendelea
kusikiliza maoni na mawazo ya
wadau na wananchi mbalimbali kuhusu namna ya
kuboresha sheria hiyo.
Hivyo, Mheshimiwa Rais Kikwete anatoa wito kwa
mwananchi yoyote mwenye maoni ama
mawazo ya namna ya kuboresha
Sheria hiyo, ajisikie yuko huru
kutoa maoni yake na Serikali
itasilikiza na kuchukua hatua zipasazo.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR
ES SALAAM.
29
Novemba, 2011