UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

 

Telephone: 255-22-2114512, 2116539

E-mail: press@ikulu.go.tz

Website:  www.mawasilianoikulu.go.tz  

Fax: 255-22-2113425

 

Description: Coat of Arms

 

PRESIDENT’S OFFICE,

      THE STATE HOUSE,

       P.O. BOX 9120,  

DAR ES SALAAM.

Tanzania.

 

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete jioni ya leo, Jumatatu, Januari 9, 2012, amekutana na kufanya mazungumzo na mjumbe maalum wa Rais wa Gambia, Mheshimiwa Yahya A. Jammeh.

 

Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika Ikulu, Dar es Salaam, mjumbe huyo maalum, Mheshimiwa Lamin Kaba ambaye pia ni Waziri wa Uvuvi, Maliasili na Masuala ya Bunge amemkabidhi Rais Kikwete ujumbe maalum kutoka kwa Rais Jammeh.

 

Katika mazungumzo yao, Rais Kikwete na Mheshimiwa Kaba wamezungumzia masuala yanayohusu uhusiano kati ya Tanzania na Gambia na pia masuala ya Afrika na ya kimataifa.

 

Mjumbe huyo maalum anatarajiwa kuondoka nchini kesho kwenda Nairobi, Kenya ambako anatarajiwa kukutana na viongozi wa nchi hiyo.

 

Imetolewa na:

 

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais,

Ikulu,

DAR ES SALAAM.

 

09 Januari, 2012