UNITED
DIRECTORATE
OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
|
Telephone:255-22-2114512, 2116898 E-mail: ikulumawasiliano@yahoo.com Fax: 255-22-2113425
|
|
PRESIDENT’S OFFICE, THE STATE HOUSE, P.O. BOX 9120, DAR ES SALAAM. Tanzania. |
TAARIFA KWA VYOMBO
VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete na ujumbe wa
serikali yake umekutana na kufanya
mazungumzo na ujumbe wa Chama cha Wananchi (CUF) ukiongozwa na Makamu Mwenyekiti
wa chama hicho, Mheshimiwa Machano Khamis Ally kuhusu namna ya
kuboresha Sheria ya Mabadiliko ya
Katiba ya Mwaka 2011.
Mkutano huo umefanyika asubuhi ya leo, Ijumaa, Desemba 2, 2011, Ikulu, mjini Dar es Salaam na ujumbe wa
CUF umemkabidhi Mheshimiwa Rais mapendekezo ya chama hicho
kuhusu namna Sheria hiyo inavyoweza
kuboreshwa.
Baada ya majadiliano ya saa mbili,
pande hizo mbili zimekubaliana kujipa nafasi ya
kutafakari zaidi na zitakutana
tena jioni ya leo.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano
ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
02
Desemba, 2011