UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

 

Telephone:255-22-2114512, 2116898

E-mail:  ikulumawasiliano@yahoo.com

press@ikulu.go.tz

Fax: 255-22-2113425

 

Coat of Arms

PRESIDENT’S OFFICE,

      THE STATE HOUSE,

P.O. BOX 9120,  

DAR ES SALAAM.

Tanzania.

 

 

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete na ujumbe wa serikali yake umekutana na kufanya mazungumzo na ujumbe wa Chama cha Wananchi (CUF) ukiongozwa na Makamu Mwenyekiti wa chama hicho, Mheshimiwa Machano Khamis Ally kuhusu namna ya kuboresha Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya Mwaka 2011.

 

Mkutano huo umefanyika asubuhi ya leo, Ijumaa, Desemba 2, 2011, Ikulu, mjini Dar es Salaam na ujumbe wa CUF umemkabidhi Mheshimiwa Rais mapendekezo ya chama hicho kuhusu namna Sheria hiyo inavyoweza kuboreshwa.

 

Baada ya majadiliano ya saa mbili, pande hizo mbili zimekubaliana kujipa nafasi ya kutafakari zaidi na zitakutana tena jioni ya leo.

 

Imetolewa na:

 

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,

Ikulu,

DAR ES SALAAM.

 

02 Desemba, 2011