DIRECTORATE
OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
UNITED
REPUBLIC OF TANZANIA
|
Telephone: 255-22-2114512, 2116898
E-mail: press@ikulu.go.tz
Fax: 255-22-2113425
|
|
PRESIDENT’S OFFICE,
THE
STATE HOUSE,
P.O. BOX 9120,
DAR
ES SALAAM.
Tanzania.
|
TAARIFA
KWA VYOMBO VYA HABARI
RAIS Jakaya Mrisho Kikwete
leo (Jumatatu,
Julai 28, 2008) amepokea hati za utambulisho
za mabalozi watatu watakaoziwakilisha nchi zao hapa
nchini.
Mabalozi hao ni
Dk. Ishaya Samaila Majanbu wa Nigeria, Japhet Isaack wa Namibia na
Brahim Salem El-Mami Buseif wa Jamhuri
ya Kidemokrasia ya Sahrawi.
Katika mazungumzo na
Balozi Majanbu Ikulu, Dar es
Salaam, mara tu
baada ya kuwa amewasilisha hati zake, Rais
Kikwete ameisifia Nigeria
kwa mchango wake mkubwa katika kutatua
migogoro katika Afrika.
“Nigeria inaendelea kutoa mchango mkubwa
katika kutafuta usuluhishi wa
mgogoro wa Darfur katika Sudan,
na pia ilichangia
kwa kiasi kikubwa katika kumaliza mapigano ya wenyewe kwa
wenyewe katika nchi za Afrika
Magharibi za Sierra Leone na Nigeria,”
amesema Rais.
Rais pia amesifia mchango
wa Rais
wa Nigeria,
Umaru Yar’Adua katika masuala mbalimbali ya kimataifa
hasa kuhusiana na utetezi wa
maslahi ya Bara la Afrika.
Rais pia amezungumzia uhusiano wa
kiuchumi unaoanza kujengeka sasa kati ya Tanzania na Nigeria kutokana na mfanyabiashara mmoja wa maarufu
wa Nigeria
kuonyesha nia dhabiti ya kuwekeza
katika ujenzi wa viwanda vya
saruji Mtwara na Mwanza.
Katika mazungumzo na Balozi
Issack wa Namibia, Rais amesifia uhusiano
imara kabisa wa kisiasa kati
ya Tanzania na Namibia na kuzitaka nchi
hizo mbili kuanza kujenga uhusiano wa kiuchumi
na ule wa
wananchi wa nchi hizo mbili.
Balozi Isaack ametaka Tanzania kuisaidia Namibia katika sekta ya utalii
na hasa
katika kupata uzoefu wa Tanzania kuhusu jinsi ya
kuwashirikisha Wanamibia wenyewe katika shughuli za utalii
ambazo kwa sasa ziko mikononi
mwa makampuni ya kigeni kwa
kiasi kikubwa.
Naye Rais Kikwete amesema
kuwa Tanzania
inahitaji kupata uzoefu wa
Namibia
katika sekta za uvuvi na
mifugo ambako nchi hiyo imepiga
hatua kubwa.
“Tunazo karibu kiasi
cha kilomita 1,000 za pwani ya bahari,
na bado
hatuna hata kiwanda kimoja cha kusindika samaki katika ukanda wa
Pwani. Kule kwenye ziwa, Ziwa
Victoria, huko uwekezaji ni mzuri kiasi
cha hata kuanza kuzuka kwa tatizo
la ukosefu wa samaki wa kutosha,”
amesema Rais.
Katika mazungumzo na
Balozi Buseif, Rais Kikwete amesisitiza
msimamo wa Tanzania wa kutaka wananchi wa Jamhuri ya
Sahrawi kupata nafasi ya kupiga kura
ya maoni kuamua hatma ya
baadaye ya nchi hiyo inayokaliwa
na Morocco.
“Msimamo wa
Tanzania haujapata
kubadilika katika kuwaunga mkono wananchi wa Sahrawi kupata nafasi ya
kuamua wenyewe hatma yao
ya baadaye, kama wanataka kuwa
huru ama wanataka kuwa sehemu
ya Morocco. Tunaunga njia ya kidemokrasia kumaliza tatizo hili. Hayo ndiyo matakwa yetu,
huo ndiyo msimamo wetu,” amesema.
Imetolea na:
Kurugenzi ya Mawasilia ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
28
Julai, 2008