DIRECTORATE
OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
UNITED
|
Telephone: 255-22-2114512, 2116898 E-mail: ikulumawasiliano@yahoo.com Fax: 255-22-2113425
|
|
PRESIDENT’S OFFICE, THE
STATE HOUSE, P.O. BOX 9120, DAR
ES SALAAM. Tanzania. |
TAARIFA
KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais JAKAYA MRISHO
KIKWETE amesema anafarijika sana kuona kauli mbinu ya CCM ya mwaka 2005 ya Maisha
Bora kwa Kila Mtanzania imetimia. “Leo miaka 5 baadae napata faraja kubwa sana
maana tumetimiza ahadi yetu”. Rais
amesema na kuongeza kuwa ukiangalia yale
yaliyofanyika kwa miaka 5 kwa ARI MPYA, KASI MPYA na NGUVU MPYA mambo mengi yamefanyika,
Rais amesema hayo leo wilayani Bunda mara baada ya kuweka jiwe la msingi kwa
ajili ya kuweka mtandao wa mabomba ya umwagiliaji katika Bwawa la Kisangwa
lilojengwa na serikali kwa shilingi milioni mia saba na ishirini na tatu na
nusu(mil.723.5).
Akifafanua azma ya Maisha Bora kwa kila Mtanzania Rais
amesema azma hiyo ina pande mbili ambazo ni mapato ya mwananchi kwa ajili ya
mahitaji yake mwenyewe na upande wa pili ni mwananchi kupata huduma za jamii
kama vile kupata maji, huduma ya afya, elimu na barabara. Bwawa la Kisangwa lina ujazo wa mita 750,000
tuta lenye urefu wa mita 8 na upana wa mita 135.
Wilaya ya Bunda sasa
ina mabwawa makubwa manne, mawili kwa umwagiliaji na mawili kwa ajili ya
matumizi ya binadamu na mifugo. Rais
ameeleza kuwa jitihada zote hizi za Serikali, ni katika kutimiza mradi wa Maendeleo
ya Kilimo na Mifugo nchini ambao unatilia mkazo matumizi ya maji katika kilimo,
matumizi ya mbegu bora, mbolea, dawa, masoko na miundombinu imara kuweza
kufikisha mazao kwa walaji. Jitihadi
hizi ndiyo zitakazowezesha maisha ya Watanzania kuinuka na kuimarika.
Wilaya ya Bunda pia
itaingizwa katika mpango wa kupewa ruzuku ya mbolea na mbegu ili kuongeza na
kukuza kilimo.
Wilaya ya Bunda pia
ina tatizo la maji safi na salama ambapo Rais amewaeleza wananchi kuwa tayari
mradi mkubwa unaofadhiliwa na Benki ya Dunia umeshaanza ambapo wilaya itapata
maji safi na salama kutoka Ziwa Victoria na pia tatizo la barabara za Bunda
zimeshafanyiwa tathmini na kuingizwa kwenye Ilani ya Uchaguzi mwaka huu na ujezi
utaanza mara moja.
Ambapo Wilaya itapata
maji safi na salama kutoka Ziwa Victoria na pia tatizo la barabara za Bunda
zimeshafanyiwa tathmini na kuingizwa kwenye Ilani ya Uchaguzi mwaka huu na
ujenzi utaanza mara moja. Rais ameondoka
Bunda na kuelekea Nansio Ukerewe, ambapo atazindua Mradi wa Umeme Vijijini.
Imetolewa
na
PREMI
KIBANGA,
Bunda,
Mara.
05/07/2010