DIRECTORATE
OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
UNITED
|
Telephone: 255-22-2114512, 2116898 E-mail: press@ikulu.go.tz Fax: 255-22-2113425
|
|
PRESIDENT’S OFFICE, THE
STATE HOUSE, P.O. BOX 9120, DAR
ES SALAAM. Tanzania. |
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Na
Mwandishi Maalum
Rais Jakaya Mrisho Kikwete amerejea nyumbani leo, Alhamisi,
Machi 19, 2009, akitokea London, Uingereza, ambako mwanzoni mwa wiki hii alihudhuria
mkutano maalum wa maandalizi ya
Mkutano wa Nchi za G-20, kuzungumzia
matatizo makubwa yanayoukabili uchumi wa dunia.
Kwenye Uwanja wa Ndege
wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar Es salaam, Rais Kikwete amelakiwa na viongozi mbali
mbali wa Serikali wakiongozwa na Waziri Mkuu
Mizengo Pinda.
Rais Kikwete alikuwa miongoni mwa viongozi wanane
wa Bara la Afrika walioalikwa na Waziri Mkuu
wa Uingereza Gordon Brown kuwakilisha msimamo wa Afrika kama
nchi za Afrika
zinavyoutaka uelezwe kwenye Mkutano wa G-20, uliopangwa kufanyika mwanzoni mwa mwezi ujao
hapo hapo London.
Viongozi wengine wa Afrika
waliohudhuria mkutano huo wa maandalizi
uliofanyika Jumatatu, Machi 16, 2009, kwenye Jumba la Lancaster House chini ya uenyekiti wa
Gordon Brown ni pamoja na Rais Khama
Ian Khama wa Botswana, na Rais Ellen Johnson Sirleaf.
Wengine ni Waziri Mkuu wa
Ethiopia Meles Zenawi, Waziri Mkuu wa
Kenya Raila
Odinga, Waziri wa Fedha wa
Afrika Kusini Trevor
Manuel, Mwenyekiti wa Tume ya Umoja
wa Afrika (AU) Jean Ping, na Rais wa
Benki ya Maendeleo ya Afrika
(AfDB) Donald Kaberuka.
Viongozi hao kwa pamoja
walimweleza Gordon Brown msimamo
wa Afrika ambao wanataka uwasilishwe katika Mkutano huo wa
G-20 ikiwa ni pamoja na:
·
Kusisitizwa kwa ukweli kuwa
Afrika kama zilivyo sehemu nyingine duniani tayari imeanza kukabiliwa na
athari na matatizo makubwa kutokana na matatizo
ya sasa ya
uchumi duniani, hata kama Bara hilo halihusiki katika kuyaanzisha matatizo hayo.
·
Kwamba katika hali hiyo Afrika
inazitaka nchi tajiri za G-8 kutenga
raslimali maalum za kulisaidia Bara la Afrika kuondokana ma matatizo hayo kwa sababu Bara la Afrika pekee halina
uwezo wa kufanya hivyo.
·
Kwamba nchi tajiri za G-20 zitimizwe ahadi zake za kulisaidia
Bara la Afrika ambazo nchi hizo zilitoa
huko nyuma lakini mpaka sasa
halizijatelekezwa. Ahadi hizo ni pamoja na zile
zilizotolewa Monterrey, Mexico na
zile zilizotolewa Gleneagles,
Scotland.
·
Kwamba makubaliano
yaliyofikiwa katika mkutano wa
aina yake uliofanyika mwezi huu mjini Dar Es Salaam, kati ya Afrika
na Shirika la Fedha Duniani (IMF) kuhusu hali ya
sasa ya matatizo
ya uchumi duniani yakubaliwe na mkutano huo
wa G-20 na yatekelezwe.
·
Kwamba Afrika inaunga mkono hatua
ya Benki ya Dunia kuanzisha
mfuko maalum wa kuzisaidia
nchi masikini zikiwamo za Afrika
kuhimili matatizo ya sasa ya
uchumi duniani.
·
Kwamba yafanyike
mageuzi makubwa katika mfumo wa
utawala wa vyombo vya fedha
duniani, ikiwamo IFM kwa lengo la kuliwezesha
shirika hilo kuwa na uwezo
mkubwa zaidi wa kusimamia uchumi
wa dunia, na pia kutoa
sauti kwa Bara la Afrika kusikika katika mfumo wa
utawala wa shirika hilo.
·
Kwamba matatizo ya sasa ya
uchumi yasiwe kisingizio cha nchi tajiri duniani kuweka vikwazo vya kujilinda zaidi
kibiashara.
·
Kwamba nchi tajiri zisitumie matatizo ya sasa
ya uchumi duniani kukata ama kupunguza misaada
yao kwa
nchi masikini za Afrika kwa
sababu kufanya hivyo kutafuta kabisa mafanikio makubwa ambayo Bara hilo limepata katika
miaka ya karibuni kutokana na kufanya mageuzi
makubwa katika chumi za nchi
za Bara hilo.
·
Kwamba kukata ama kupunguza misaada
pia kutazifanya nchi za Afrika
kushindwa kufikia Malengo ya Milenia,
ambayo shabaha yake kuu ni kupunguza umasikini duniani kwa asilimia 50.
Mbali na
kuhudhuria mkutano huo, akiwa London, Rais pia alikutana
na watu mbali
mbali akiwamo Waziri Mkuu wa
Kenya, Odinga na Waziri wa Misaada
ya Kimataifa ya Maendeleo wa
Uingereza, Douglas Alexander.
Akiwa njiani kurejea nyumbani kutoka London, Rais Kikwete na
ujumbe wake ulisimama kwa siku moja
Dubai kwa shughuli nyingine za kikazi.
Mwisho.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais
Ikulu.
Dar es Salaam.