UNITED
DIRECTORATE
OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
|
Telephone: 255-22-2114512, 2116898 E-mail: press@ikulu.go.tz Fax: 255-22-2113425
|
|
PRESIDENT’S OFFICE, THE STATE HOUSE, P.O. BOX 9120,
DAR ES SALAAM. Tanzania. |
TAARIFA KWA VYOMBO
VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Aidha, Rais Kikwete amesema kuwa hakuna urithi
bora zaidi ambao mzazi yoyote
anaweza kutoa kwa mtoto
wake kuliko kumpa elimu.
Rais Kikwete ameeleza hayo, usiku wa
jana, Alhamisi 29, 2010, wakati wa chakula
cha usiku cha kuchangisha fedha za ujenzi
wa shule ya sekondari ya
Ebenezer Lutheran Junior Seminary ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT), Dayosisi ya Morogoro, kwenye
ukumbi wa CCT mjini Morogoro.
Akizungumza kabla ya kuanza
kwa uchangiaji,
Rais Kikwete aliwaambia washiriki wa chakula hicho
cha jioni: “Jitihada mnayofanya ya kupanua
elimu kwa kujenga shule ni
kielelezo tosha cha jinsi gani viongozi
wetu wa dini
mnavyojali maendeleo ya waumini wenu
na wananchi kwa jumla.”
Aliongeza Mheshimiwa Rais Kikwete: “Sote tunatambua kuwa elimu ni ufunguo
wa maisha. Hakuna urithi wenye thamani
zaidi unaoweza kumpatia mtoto kuliko elimu. Nawapongezeni
Akimkaribisha Mheshimiwa Rais, Askofu Jacob Mameo Ole Paulo, Askofu wa
Dayosisi ya Morogoro, alipongeza mafanikio ya Serikali
ya Awamu ya Nne kwa
mafanikio makubwa katika miaka mitano
iliyopita:
“Mmepambana na
rushwa na madawa ya kulevya.
Mmepanua
Askofu Ole Paulo alisema
kuwa Dayosisi ya Morogoro ambayo
ni moja
ya dayosisi 20 za KKKT Tanzania nzima imeamua kujenga shule ya sekondari
kwa sababu kwa sasa haina
hata shule moja ya sekondari.
Alisema kuwa shule hiyo
ya Ebenezer Lutheran Junior Seminary itakuwa ya mkondo
wa sayansi
na itaanza kwa kidato cha tano na sita
kabla ya kuanza kwa kidato
cha kwanza hadi cha nne na kuwa ujenzi
utagharimu sh bilioni 2.41.
Askofu huyo ameishukuru Serikali kwa kulipatia
dayosisi hiyo ekari 47 kwa ajili
ya ujenzi wa shule hiyo
na ahadi ya kuongezewa ekari
nyingine 53 ili kufikisha ekari 100.
Katika mchango wa jana,
kiasi cha sh 131, 825,000 zilipatikana
zikiwamo sh milioni 22 taslimu na kiasi
kingine 46 kilikwishakuchangwa
kabla ya hafla hiyo.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
30 Julai, 2010