DIRECTORATE
OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
UNITED
|
Telephone: 255-22-2114512, 2116898 E-mail: ikulumawasiliano@yahoo.com Fax: 255-22-2113425
|
|
PRESIDENT’S OFFICE, THE
STATE HOUSE, P.O. BOX 9120, DAR
ES SALAAM. Tanzania. |
Rais
Jakaya Mrisho Kikwete ameagiza uongozi wa Shirika la Umeme Tanzania TANESCO
kusimamia shughuli ya kutengeneza mashine zilizoharibika katika kituo cha umeme
cha Lizaboni, mjini Songea kwa karibu zaidi ili wananchi waondokane na tatizo
la ukosefu wa umeme linalowakabili kwa kipindi kipatacho miezi minne sasa.
Rais
Kikwete ametoa maagizo hayo leo mara baada ya kukagua kituo hicho cha TANESCO
na kukutana na wananchi wengi waliokuwa wanamlilia kuwatafutia ufumbuzi wa
umeme ambao umekuwa kero kubwa kwao.
“Simamieni
kwa karibu matengenezo ya mashine hizi ili tofauti ianze kuonekana baada ya
siku nne” amesema.
Kulingana
na taarifa za TANESCO katika mji wa Songea, mashine mbili kati ya sita
zinazozalisha umeme katika mji huo zimeharibika na ziko katika hatua ya mwisho
ya matengenezo na wamemweleza Rais kuwa kifaa kinachotakiwa katika machine moja wapo kimeshaletwa na
kufungwa ila wanasubiri mafundi kutoka kampuni ya Caterpillar waje kusimamia
kuanza kwa uzalishaji wa umeme katika mashine moja wapo. Hata hivyo kifaa
kingine kitachukua zaidi ya majumu mawili kwani kinahitaji matengenezo zaidi.
Rais
Kikwete amesema hii ni hatua ya dharura kwa sasa kwani mji huo umo katika
mpango wa baadaye wa kupata umeme kutoka katika grid ya Makambako ambayo
itachukua muda mrefu.
Rais
Kikwete amefika kituoni hapo akitokea Wilaya ya Namtumbo ambako alikwenda
kukagua shughuli za maendeleo, kuhamasisha
na kufungua miradi ya wananchi ambapo amekamilisha ziara yake kwa
kufungua ofisi ya mkuu wa Wilaya.
Akiwa
katika Wilaya ya Mbinga na Namtumbo, Rais amesikiliza kero za wananchi kupitia
kwa viongozi wao ambapo kero kubwa zimekua zinazohusu maji, afya, elimu na
Kilimo.
Akijibu
hoja za matatizo hayo, Rais ameelezea hatua mbalimbali na juhudi zinazofanywa
na serikali katika kutatua matatizo hayo.
Katika
elimu suala kubwa limekuwa shule, walimu na maabara, Rais amesema suala la
walimu ni suala ambalo serikali inalifahamu na hivi karibuni walimu watahitimu
na kuajiriwa katika shule zilizojengwa kwani serikali ilichukua hatua ya
makusudi ya kuongeza vyuo vya elimu nchini vikiwemo vyuo vya Chang’ombe, mkoani Dar-Es-Salaam, Mkwawa cha
Mkoani Iringa na Chuo Kikuu cha
Rais
pia amesema kuanzia mwaka ujao serikali, kwa kushirikiana na Benki ya Maendeleo
ya Afrika (ADB) na Benki ya Dunia itaanza
mpango mkubwa wa kujenga maabara kwa ajili ya shule zote hapa nchini. Rais
amerejea Dar-Es-Salaam leo jioni.
Mwisho
Imetolelwa
na Premi Kibanga
Ikulu.
13 Agosti, 2009