DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

 

Telephone: 255-22-2114512, 2116898

E-mail: press@ikulu.go.tz             

Fax: 255-22-2113425

 

 

PRESIDENT’S OFFICE,

      THE STATE HOUSE,

       P.O. BOX 9120,  

DAR ES SALAAM.

Tanzania.

 

 

 

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Bi. Zahra Mwanasharif Nuru kuwa Msaidizi wa Rais wa masuala ya Diplomasia.

 

Taarifa iliyotolewa leo, Jumatano, Julai 15, 2009 na Katibu Mkuu Ikulu, Ndugu Michael Mwanda, kwa niaba ya Katibu Mkuu Kiongozi, inasema kuwa uteuzi huo ulianzia juzi, Jumatatu, Julai 13, 2009.

 

Taarifa hiyo inasema kuwa Bi Zahra Nuru anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Balozi Andrew M. Daraja ambaye alihitimisha mkataba wake wa utumishi wa umma.

 

Bi. Zahra Nuru amepata kuajiriwa na Umoja wa Mataifa. Kabla ya kuhitimisha mkataba wake na Umoja wa mataifa, Ndugu Zahra Nuru alikuwa Mtaalam na Mshauri Mwandamizi wa Katibu Mkuu Msaidizi na Mshauri Maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu Afrika (Consultant and Senior Adviser to the Under Secretary-General and UN Special Adviser on Africa).

 

Imetolewa na:

 

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,

Ikulu,

DAR ES SALAAM.

 

15 Julai, 2009