DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

 

Telephone: 255-22-2114512, 2116898

E-mail:  ikulumawasiliano@yahoo.com

              press@ikulu.go.tz             

Fax: 255-22-2113425

 

PRESIDENT’S OFFICE,

      THE STATE HOUSE,

       P.O. BOX 9120,  

DAR ES SALAAM.

Tanzania.

 

 

 

Rais Jakaya Mrisho Kikwete amemtumia salamu za pongezi Prof. Anna Tibaijuka, Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Makazi la Umoja wa Mataifa, United Nations Human Settlements Programme (HABITAT) kwa kutunukiwa tuzo ya Mazingira ya Goteborg  kwa mwaka 2009 (2009 Goteborg Award, the prestigious “Nobel Prize in Environment).

 

Rais Kikwete amemweleza Prof Tibaijuka kuwa tuzo hii inaonesha kuwa dunia nzima inatambua uongozi wake na mafanikio katika kuendeleza makazi ya kudumu duniani.

 

Sifikiriii mtu mwingine ambaye anastahili tuzo hii yenye fahari kubwa, ni wazi kwamba, jopo lililokuchagua limechagua vemaamesema na kumuelezea kuwa tuzo hii imeleta fahari kubwa si kwa kwake tu ila kwa taifa zima la Tanzania, kama mtanzania na balozi wake.

 

Kila Mtanzania anajivunia mafanikio yako na wanaungana nami kukutumia salaam hizi za pongezi, kwa mara ingine umetufanya sisi sote tutembea kifua mbele, nakutakia afya njema na mafanikio lukuki katika yote unayotarajia kufanya”. Rais amemwambia Prof. Tibaijuka.

 

Prof Tibaijuka amepata Tuzo hiyo kwa pamoja na wenzie wawili ambao ni Bw. Enrique Penalosa wa Colombia na Bw. Soren Hermansen wa Denmark.

 

Mwisho

 

Imetolewa na:

Premi Kibanga, Mwandishi wa Rais, Msaidizi,

Ikulu-Dar-es-Salaam

16 Julai, 2009