DIRECTORATE
OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
UNITED
|
Telephone: 255-22-2114512, 2116898 E-mail: press@ikulu.go.tz Fax: 255-22-2113425
|
|
PRESIDENT’S
OFFICE, THE STATE HOUSE, P.O. BOX 9120,
DAR ES SALAAM. Tanzania. |
TAARIFA
KWA VYOMBO VYA HABARI
SALAMU ZA
RAMBIRAMBI ZA MWENYEKITI WA CCM – TAIFA NA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA
Mwenyekiti
wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) – Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Marehemu
Jidulamabambasi alikuwa miongoni mwa wanachama wa CCM waliokuwa wamejitokeza
kuwania kuteuliwa na Chama Cha Mapinduzi kugombea Ubunge katika Jimbo la
Uchaguzi la Maswa Magharibi.
“Ninakutumia
salamu za rambirambi wewe Katibu Mkuu wa CCM na wana – CCM kote nchini kwa
kumpoteza mmojawapo wa makada katika chama chetu”, amesema Mhe. Kikwete katika salamu zake, na
kuongeza, “aidha kupitia kwako, natuma salamu za rambirambi na pole nyingi kwa
familia ya marehemu Amani Nzugile Jidulamabambasi kwa kuondokewa na kiongozi
muhimu wa familia
Katika
salamu hizo za rambirambi, Mhe. Kikwete amemwelezea marehemu kuwa miongoni mwa
makada jasiri wa CCM wasiokata tamaa katika medani za siasa na mpambanaji
hodari aliyekuwa na dhamira ya dhati ya kulitumikia Taifa na Umma wa Watanzania
hususan wananchi wa Jimbo la Maswa Magharibi kupitia tiketi ya Chama Cha
Mapinduzi.
Amesema
anamwomba Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema aiweke mahali pema peponi roho ya
Marehemu Jidulamambasi na kuwaomba wafiwa pamoja na ndugu, jamaa na marafiki
kuwa na moyo wa uvumilivu na subira wakati huu wa maombolezo kwani yote ni
mapenzi yake Mola.
Imetolea na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR
ES SALAAM.
03 Agosti, 2010