UNITED
DIRECTORATE
OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
|
Telephone: 255-22-2114512, 2116539 E-mail: press@ikulu.go.tz Website: www.mawasilianoikulu.go.tz Fax: 255-22-2113425
|
|
PRESIDENT’S OFFICE, THE
STATE HOUSE, P.O. BOX 9120, DAR
ES SALAAM. Tanzania. |
TAARIFA
KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo, Ijumaa, Machi 11,
2011 amekutana na kufanya mazungumzo na wafanyabiashara wazito kutoka nchi za
Japan na Uturuki.
Katika mikutano
hiyo miwili tofauti iliyofanyika Ikulu, Dar es Salaam, Rais Kikwete kwanza
amekutana na wajumbe wa Kamati ya Mahusiano ya Africa-Japan ya Chama cha
Watendaji Waandamizi wa Makampuni ya
Japan cha Keizai Doyukai.
Kundi hilo la
wafanyabishara kutoka Japan liliongozwa na
Bwana Sekiyama Mamoru, Mwenyekiti
wa Kamati hiyo ambaye pia ni Makamu wa Rais wa Bodi ya Kampuni ya Marubeni
Corporation.
Baadaye, Rais
Kikwete amekutana na kuzungumza na kundi la wafanyakabiashara ya Uturuki
wakiongozwa na Waziri wa Nchi wa Biashara wa Serikali ya Uturuki, Mheshimiwa
Zafer Caglayan.
Rais Kikwete
amewataka Wajapan hao wanaotembelea nchi za Tanzania, Kenya na Ethiopia
kuongeza kasi yao katika kuwekeza katika uchumi wa Tanzania na hasa katika
maeneo ya uzalishaji umeme, kilimo, uvuvi, usafirishaji wa mizigo na uchimbaji
wa madini.
Aidha, Rais
Kikwete, kupitia kwa ujumbe huo kutoka Japan, ametoa rambirambi na pole kwa
nchi ya Japan na wananchi wake kufuatia tetemeko kubwa la ardhi lilisababisha
tsunami kwenye pwani ya nchi hiyo.
Kiasi cha watu kati
ya 200 na 300 wanaripotiwa kupoteza maisha katika tsunami hiyo ambayo pia
imesababisha kiasi cha mioto 80 katika sehemu mbalimbali za Japan ukiwemo moto
uliolipuka katika kiwanda cha kusafisha mafuta.
Katika mazungumzo
na Waziri Caglayn na ujumbe wake, Rais
Kikwete amerudia wito ule ule wa kuwakaribisha wafanyabiashara na makampuni ya
Uturuki kuja kuwekeza Tanzania. Ujumbe huo ulikuwa nchini kwa mkutano na
wafanyabiashara wa Tanzania.
Waziri huyo wa
Uturuki pia amewasilisha kwa Rais Kikwete ujumbe maalum kutoka kwa Rais wa
Uturuki, Mheshimiwa Abdullah Gur na mwaliko wa kumwomba ahudhurie mkutano wa
nchi zenye maendeleo kidogo zaidi wa LDC ulipangwa kufanyika nchini Uturuki Mei
mwaka huu.
Mwisho.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
11 Machi, 2011