UNITED REPUBLIC OF
TANZANIA
DIRECTORATE OF
PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
|
Telephone: 255-22-2114512, 2116539 E-mail: press@ikulu.go.tz Website: www.mawasilianoikulu.go.tz Fax: 255-22-2113425
|
|
PRESIDENT’S
OFFICE, THE STATE HOUSE, P.O. BOX
9120, DAR ES SALAAM. Tanzania. |
TAARIFA KWA VYOMBO
VYA HABARI
Rais wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete
leo, Jumatatu, Juni 6, 2011, amekutana na kufanya mazungumzo
na Waziri wa Utamaduni, Michezo
na Utalii wa Jamhuri ya
Korea, Mheshimiwa Dkt. Choung Byoung Gug.
Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika Ikulu, Dar es Salaam, viongozi hao wawili wamezungumzia
uhusiano kati ya Tanzania na
Korea na ushirikiano baina ya nchi
hizo mbili katika Nyanja mbalimbali.
Miongoni mwa mambo mengine, Mheshimiwa Gug amemwelezea Rais Kikwete mipango ya nchi hiyo
ya kutaka kuitangaza Mbuga ya Wanyama ya
Serengeti ili kuweza kuvutia watalii zaidi wa
Korea kutembelea Tanzania.
Mheshimiwa Gug pia amemwelezea
Rais Kikwete kuhusu mipango ya nchi hiyo
ya kuisaidia Tanzania katika kujenga maktaba katika shule za
msingi hasa katika mikoa ya
Dar es Salaam na
Pwani na kuwafundisha walimu namna bora zaidi
ya kutumia maktaba hizo.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
06
Juni, 2011