DIRECTORATE
OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
UNITED
|
Telephone: 255-22-2114512, 2116898 E-mail: press@ikulu.go.tz Fax: 255-22-2113425
|
|
PRESIDENT’S OFFICE, THE
STATE HOUSE, P.O. BOX 9120, DAR
ES SALAAM. Tanzania. |
TAARIFA
KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais Kikwete apokea ripoti ya awali ya milipuko
ya Mlima Oldonyo Lengai
Rais Jakaya Mrisho
Kikwete jana, Jumatano, Januari 28, 2009, alipokea ripoti ya awali ya milipuko
ya mara kwa mara ya jivu la volkano kutoka kwenye kwenye Mlima wa Oldonyo Lengai katika Mkoa wa
Arusha kutoka kwa watalaam wa masuala ya volkano wa Marekani.
Ripoti hiyo
iliwasilishwa kwa Rais Kikwete na Mshauri wa Sayansi ya Miamba kutoka Ofisi ya
Mpango wa Marekani wa Misaada ya Nje ya Maafa (VDAP) cha Mamlaka ya Maendeleo
ya Kimataifa, Gari Mayberry wakati mtaalam huyo alipokutana na kufanya mazungumzo
na Rais. Ikulu,
Maybeery alimwambia
Rais Kikwete kuwa ripoti hiyo ni ya awali tu na uchunguzi zaidi utahitaji
kuweza kuthibitisha baadhi ya mambo ambayo yamegunduliwa katika uchunguzi huo
wa awali.
VDAP ilifanya
uchunguzi huo kuhusu milipuko ya mara kwa mara ya volkano katika Mlima Oldonyo
Lengai kufuatia ombi la Serikali ya
Ripoti hiyo ya
awali imegundua masuala matano kuhusu milipuko hiyo na inatoa mapendekezo ya
aina mbili – manane ya muda mfupi na mawili ya muda mrefu.
Mlima wa Oldonyo
Lengai ulioko chini ya Mamlaka ya Eneo la Hifadhi la Ngorongoro (NCCA)
ulilipuka mara kwa mara hasa mwaka juzi na kufuatia hali hiyo, Serikali ya
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR
ES SALAAM.
29 Januari, 2009