DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

 

Telephone: 255-22-2114512, 2116898

E-mail: ikulumawasiliano@yahoo.com

press@ikulu.go.tz              

Fax: 255-22-2113425

 

Coat of Arms

PRESIDENT’S OFFICE,

      THE STATE HOUSE,

       P.O. BOX 9120,  

DAR ES SALAAM.

Tanzania.

 

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais Jakaya Mrisho Kikwete amemtumia salamu za Rambirambi Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania, Bibi Sophia Simba, kufuatia kifo cha mmoja wa wanachama wake hodari Bibi Rhoda Kahatano aliyefariki usiku wa kuamkia leo nyumbani kwake Bunju A, jijini Dar-Es-Salaam.

Katika salamu hizo Rais Kikwete amesema amemfahamu na kufanya naye kazi katika chama na serikali na kumuelezea kuwa mwananchama dhabiti, aliyeshirikiana vyema na wenzake na muwajibikaji mkubwa.

Alikwua  nguzo imara katika kusimamia masuala ya chama na serikali na muwajibikaji ambaye anakumbukwa wakati wote  kwa ushirikiano na upendo mkubwa kwa wenzake siku zote”. Rais amesema

Tutamkumbuka kwa kupenda kutoa ushauri, ushirikiano, upendo na ucheshi kwa watu wote na wakati woteRais amesema na kumuomba Mwenyekiti wa UWT, amfikishie rambirambi zake kwa Mume, watoto na wana familia ya Marehemu Rhoda Kahatano kwa kuondokewa na mpendwa wao.

Marehemu Rhoda Kahatano alizaliwa Tukuyu, Mbeya tarehe 15 Desemba, 1941.  Aliwahi kuwa Mkuu wa Wilaya mkoani Kagera kabla ya kuwa Mbunge wa Viti Maalum kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutoka mwaka 1995 hadi 2000.

Amekuwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM na  Mjumbe wa UWT katika kipindi cha uhai wake.

Ameacha mume, watoto na wajukuu.

 

Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,

Ikulu.

Dar es Salaam.

18 Agosti, 2010