DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
UNITED
|
Telephone: 255-22-2114512, 2116898 E-mail: ikulumawasiliano@yahoo.com Fax: 255-22-2113425
|
|
PRESIDENT’S OFFICE, THE STATE HOUSE,
P.O. BOX 9120,
DAR ES SALAAM. Tanzania.
|
TAARIFA
KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais Jakaya Mrisho Kikwete leo
mchana amepokea ripoti za Ukaguzi wa Matumizi
ya Fedha za Serikali na Taasisi zake za mwaka 2008/2009 kutoka kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu
za Serikali Bwana Ludovick Utouh.
Ripoti alizopokea Rais ni za Ukaguzi
wa Taarifa za Fedha ambazo zinahusu Serikali Kuu, Serikali za Mitaa na za Mashirika
ya Umma.
Ripoti zingine ni za Ufanisi
ambazo ni ripoti ya jumla ya Ukaguzi wa Ufanisi, ukaguzi wa ufanisi na thamani
ya Fedha kwenye sekta ya ujenzi wa Barabara.
Kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri
ya Muungano wa
Katika mazungumzo hayo Bwaba
Utouh amemueleza Rais Kikwete juu ya mafanikio mbalimbali ya Ukaguzi wa Hesabu
za Serikali kutoka mwaka 2005/2006 hadi za 2008/2009 na kuonyesha kuridhishwa
nazo.
Baadhi ya mafanikio hayo ni
uwezo wa ofisi yake kuwakilisha ripoti 4 kwa mwaka huu 2008/2009 kutoka ripoti
2 mwaka uliopita wa 2005/2006.
Itakumbukwa kuwa Ripoti za mwaka 2005/2006 zilijadiiwa chini ya Uenyekiti
wa Rais Kikwete katika vikao muhimu vitatu ambacho ni kikao cha Baraza la
Mawaziri, Kikao cha viongozi wakuu wa
Serikali Kuu kilichofanyika na kikao cha
Viongozi Wakuu wa Serikali za Mitaa vyote vilifanyika Aprili , 2007.
Bwana Utouh pia ameeleza kuwa
tofauti na ripoti za mwaka 2005/2006 ambazo uandaaji wa taarifa za Serikali Kuu
na Serikali za Mitaa ulitumia viwango na miongozo ya ndani ya nchi, uandaaji wa
ripoti hizi mpya umetumia viwango vya kihasibu vya Kimataifa.
Hatua nyingine kubwa
iliyofikiwa na ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ni kuwa
ukaguzi wa Balozi za Tanzania za ripoti iliyopita ulifanyika kwa kutumia
sampuli chini ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, wakati
ripoti hii ya leo ukaguzi umefanyika kwa Balozi zote na kila Balozi kupewa hati
yake ya Ukaguzi na katika ukaguzi mzima hati za mwaka huu zinaonyesha kuboreka
zaidi kuliko za kipindi kilichopita.
Akipokea Ripoti hizo Rais
Kikwete ameishukuru ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa
kazi hiyo na kuahidi kuijengea ofisi hiyo ili ifanye kazi vizuri zaidi.
“ Tutafanya jitihada ya kuwawezesha
zaidi, ni muhimu kuongeza watumishi, mishahara, vitendea kazi ili mfanye kazi
vizuri zaidi”. Amesema Rais na kusisitiza kuwa nidhamu kwenye matumizi
ya fedha ni muhimu na kwamba tangu serikali ilipoelezea na kukuza uelewa na
umuhimu wa nidhamu katika matumizi ya fedha kwa viongozi na watendaji, nidhamu
imeanza kuonekana na hivyo hakuna budi kujenga nidhamu zaidi.
Mwisho
Imetolewa na Premi Kibanga,
Mwandishi wa Habari wa Rais,
Msaidizi,
Ikulu
Dar-Es-Salaam.
31 Machi, 2010