UNITED REPUBLIC OF
TANZANIA
DIRECTORATE OF
PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
|
Telephone: 255-22-2114512, 2116539 E-mail: press@ikulu.go.tz Website: www.mawasilianoikulu.go.tz Fax: 255-22-2113425
|
|
PRESIDENT’S
OFFICE, THE STATE HOUSE, P.O. BOX
9120, DAR ES SALAAM. Tanzania. |
TAARIFA KWA VYOMBO
VYA HABARI
Rais Jakaya Mrisho Kikwete
amewaandikia barua Waziri Mkuu na
Waziri wa Fedha kuwataka kuziwakilisha bungeni ifikapo tarehe 12 Aprili, mwaka huu
ripoti za Mkaguzi Mkuu wa
Serikali juu ya Hesabu
za Serikali za Mitaa, Hesabu
za Serikali Kuu, za Mashirika ya Umma
na Ukaguzi wa Ufanisi kwa
mwaka 2009/10 kama ilivyo kikatiba.
Tayari Mkaguzi Mkuu ameziwakilisha
ripoti hizi kwa Rais, jana
mchana (29 Machi, 2011) kama ilivyo kwa mujibu wa
Katiba ya Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania ya mwaka 1977, iliyorekebishwa mwaka 2005, kifungu cha 28 cha Sheria ya Ukaguzi
wa Umma namba
11 ya mwaka 2008.
Kwa Mujibu wa Sheria
Ripoti hizi zinatakiwa kuwakilishwa kwa Rais kabla
ya tarehe ya mwisho wa
mwezi wa Machi, na Rais
anatakiwa kuwaandikia mawaziri wanaohusika mapema iwezekanavyo ili kuweza kuwasilishwa
kwenye kikao cha bunge linalofuata baada ya hapo.
Ripoti hizo zinahusu ukaguzi
wa fedha
za Serikali za Mitaa, Serikali
Kuu na za
Mashirika ya Umma. Ripoti pia
zimekagua ufanisi wa utendaji wa
Wizara ya Miundombinu na TANROADS katika kusimamia na ujenzi wa
barabara nchini.
Ripoti zimebainisha kuwa bado kuna mapungufu
na changamoto nyingi ambazo zinahitaji
kurekebishwa na pia Mkaguzi Mkuu
ametoa mapendekezo muhimu ambayo yanalenga
katika udhibiti na matumizi bora
ya fedha na rasilimali za
nchi hii ambayo Rais ameyaafiki.
Rais amemshukuru na kumpongeza Mkaguzi Mkuu, Bw. Ludovick
Utouh kwa kazi yake nzuri
na makini na kumtaka aendelee
na kuwachukulia hatua wale wote wanaokiuka taratibu na kutumia fedha
za Umma vibaya na kueleza kuwa lazima
viongozi na watumishi wa serikali
kuzingatia taratibu zilizopo na kutambua
kuwa serikali haiwezi kuendeshwa kama haikusanyi mapato yake vizuri.
Mwisho.
Imetolewa na:
Premi Kibanga,
Mwandishi wa Habari
wa Rais Msaidizi,
Ikulu,
DAR
ES SALAAM
30
Machi, 2011