DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

 

Telephone: 255-22-2114512, 2116898

E-mail: press@ikulu.go.tz             

Fax: 255-22-2113425

 

 

PRESIDENT’S OFFICE,

      THE STATE HOUSE,

       P.O. BOX 9120,  

DAR ES SALAAM.

Tanzania.

 

 

 

 

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

 

SALAMU ZA RAMBIRAMBI ZA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA JAKAYA MRISHO KIKWETE KUTOKANA NA KIFO CHA MBUNGE WA RUANGWA (CCM), MHESHIMIWA SIGIFRID NG’ITU

 

          Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemtumia salamu za rambirambi Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samuel Sitta (MB) kutokana na kifo cha Mbunge wa Ruangwa kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM); Mheshimiwa Sigifrid Ng’itu.

 

          Marehemu Sigifrid Ng’itu alifariki dunia usiku wa kuamkia tarehe 2 Novemba, 2009 katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) alikokuwa amelazwa.

 

          “Ni kwa masikitiko na majonzi makuu, ninakutumia salamu za rambirambi kutokana na kifo cha Mbunge wa Jimbo la Ruangwa kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Marehemu Sigifrid Ng’itu……kifo hicho kwa hakika ni pigo kubwa kwa familia ya marehemu, Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wananchi wa Jimbo la Ruangwa na Taifa kwa ujumla”, amesema Rais Kikwete katika salamu zake.

 

          Rais Kikwete amemuelezea Marehemu Sigifrid Ng’itu kama kiongozi aliyekuwa na mchango mkubwa kutokana na jinsi alivyokuwa mstari wa mbele kuwaletea maendeleo wananchi wa Jimbo lake la Ruangwa na jinsi alivyokuwa anawatetea ndani ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

 

          Rais Kikwete ameitaka familia, ndugu, jamaa na marafiki wa Marehemu Sigifrid Ng’itu kuwa na moyo wa uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo na kumuomba Mwenyezi Mungu ailaze roho ya Marehemu mahali pema peponi.

 

Imetolewa na:

 

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,

Ikulu,

DAR ES SALAAM.

 

05 Novemba, 2009