DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

 

Telephone: 255-22-2114512, 2116898

E-mail: press@ikulu.go.tz             

Fax: 255-22-2113425

 

 

PRESIDENT’S OFFICE,

      THE STATE HOUSE,

       P.O. BOX 9120,  

DAR ES SALAAM.

Tanzania.

 

 

 

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

 

SALAMU ZA RAMBIRAMBI ZA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHE. JAKAYA MRISHO KIKWETE

 

            Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemtumia salamu za rambirambi Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Abbas Kandoro kutokana na vifo vya wanafunzi 18 waliozama katika Ziwa Victoria, baada ya mtumbwi waliokuwa wakisafiria kutoka kijijini kwao Lukumbi, Kata ya Chifunfu, Tarafa ya Katunguru wilayani Sengerema kuzama leo asubuhi tarehe 5 Agosti, 2010.

 

            Kutokana na ajali hiyo ya kusikitisha ambayo imetupotezea maisha ya vijana waliokuwa wanahitajika sana kwa maendeleo ya Taifa letu, ninakutumia salamu za rambirambi wewe Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, na kupitia kwako natuma salamu za rambirambi na pole nyingi kwa familia za wafiwa”,  amesema Rais Kikwete katika salamu zake.

 

            Rais Kikwete amesema anawahakikishia wafiwa wote kuwa yupo pamoja nao katika msiba huo mkubwa, kwa kutambua kwamba wapo katika majonzi makubwa na anamuomba Mwenyezi Mungu aziweke mahali pema peponi roho za marehemu wote.

 

            Hata hivyo amewaomba wawe na moyo wa uvumilivu na ujasiri katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo ya vijana wao.

 

Imetolewa na:

 

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,

Ikulu,

DAR ES SALAAM.

 

05 Agosti, 2010