UNITED
DIRECTORATE
OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
|
Telephone: 255-22-2114512, 2116539 E-mail: press@ikulu.go.tz Website: www.mawasilianoikulu.go.tz Fax: 255-22-2113425
|
|
PRESIDENT’S OFFICE, THE STATE HOUSE, P.O. BOX 9120,
DAR ES SALAAM. Tanzania. |
TAARIFA KWA
VYOMBO VYA HABARI
SALAMU za rambirambi kwa
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete kufuatia ajali ya kuzama
kwa meli ya Spice Islander na kuua watu 202 zimezidi
kumiminika nchini kutoka Jumuia ya
Kimataifa.
Salamu hizo za rambirambi
pia zimetumwa kwa Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti
wa Baraza la Mapinduzi
Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein.
Hadi leo, Jumatano, Septemba 14, 2011, Mheshimiwa Rais
Kikwete alikuwa ametumiwa salamu za rambirambi kutoka
sehemu mbalimbali 22, zikiwemo zile kutoka
kwa Mfalme wa Sweden Mfalme Carl Gustaf R, Gavana Mkuu wa Canada Mheshimiwa David Johnston, Waziri Mkuu wa Mauritius Mheshimiwa Dkt.
Navinchandra Ramgoolam na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Mheshimiwa
Ban Ki Moon.
Salamu nyingine zimepokelewa kutoka nchi za
Benin, Philippines, Ukraine, Poland, Belarus, Misri, na Khazkistan.
Aidha, salamu nyingine zimetumwa kwa Mheshimiwa Rais Kikwete kutoka
kwa Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Mama Asha
Rose Migiro, Mkuu wa Mkoa
wa Kagera Mheshimiwa Mohammed Babu,
Balozi wa Tanzania katika Ufaransa Mama Begum Karim Taj, na Balozi
wa Tanzania katika nchi za Misri Mheshimiwa Ali Shauri Haji ambaye pia anaiwakilisha Tanzania katika Israel, Jordan, Libya, Lebanon, Syria na Palestine.
Mheshimiwa Rais
Kikwete pia amepokea salamu za rambirambi kutoka
kwa Kaimu
Balozi wa Tanzania katika Oman Mheshimiwa Abdallah Abasi Kilima, Balozi
wa Tanzania katika India Mhandisi
John H. Kijazi, Balozi wa
Tanzania katika Canada Mheshimiwa
Alexander C. Masinda na Balozi wa Tanzania katika Brazil
Mheshimiwa Francis Malambugi.
Salamu pia zimepolekewa kutoka kwa
Katibu Mtendaji wa International
Conference on the Great Lakes Region Balozi Liberata Mulamula na kutoka kwa
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa
Mazao (Common Fund for Commodities), Mheshimiwa Ali Mchumo.
Meli ya Spice Islander ilizama kwenye pwani ya
Zanzibar katika eneo la Nungwi usiku wa kuamkia Jumamosi, Septemba 10, mwaka huu, 2011 na mpaka
sasa watu 202 wamethibitishwa kuwa walipoteza maisha katika ajali hiyo
na wengine 619 waliokolewa katika ajali hiyo.
Hadi sasa meli hiyo
iliyokuwa inasafiri kutoka Dar es Salaam kwenda Pemba kupitia Zanzibar haijaweza kuopolewa kutoka
baharini hata kama wazamiaji wa ndani na kutoka
Afrika Kusini wanaendelea na kazi ya kuitafuta
meli hiyo.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR
ES SALAAM.
14
Septemba, 2011