UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

 

Telephone: 255-22-2114512, 2116898

E-mail: press@ikulu.go.tz             

Fax: 255-22-2113425

 

 

PRESIDENT’S OFFICE,

      THE STATE HOUSE,

       P.O. BOX 9120,  

DAR ES SALAAM.

Tanzania.

 

 

 

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, ametuma rambirambi kwa Balozi Mstaafu Andrew Daraja kufuatia mauaji ya mkewe balozi huyo, Mama Anna Daraja, yaliyotokea mwishoni mwa wiki.

 

Katika rambirambi zake, leo, Jumanne, Machi 9, 2010, Rais Kikwete amesema kuwa ameshitushwa mno na kuhuzunishwa na mauaji ya mama huyo, aliyekuwa na umri wa miaka 65, yaliyotokea katika mazingira ambayo hajafafanuliwa.

 

“Nimepokea kwa majonzi na huzuni nyingi kifo cha Mama Anna Daraja. Nilipata kumfahamu binafsi Mama Daraja. Alikuwa mtu mwema na mpenda watu.” Amesema Rais Kikwete katika rambirambi hizo na kuongeza:

 

“Napenda kwa dhati ya moyo wangu kukutumia wewe, ndugu Andrew Daraja pamoja na familia yako yote, ndugu na jamaa zako wote, rambirambi zangu za moyoni kabisa kutokana na kifo hiki cha ghafla.”

 

Ameongeza Mheshimiwa Rais: “Mawazo yangu na ya familia yangu, yako nanyi katika kipindi hiki kigumu cha kuondokewa ghafla na mpendwa wenu. Namwomba Mwenyezi Mungu awapewani nguvu na subira kuweza kuwa na uvumilivu wa kuvuka kipindi hiki. Ni mapenzi yake Mwenyezi Mungu.”

 

Balozi Daraja alistaafu utumishi wa Serikali Septemba 2007, baada ya kuwa ametumikia katika nafasi mbalimbali, ikiwa ni pamoja na kuwa Balozi wa Tanzania katika nchi za Ujerumani na Marekani.

 

Pia Balozi daraja alipata kuwa mwandishi wa hotuba, na baadaye kuwa mshauri wa masuala ya kibalozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika utumishi wake.

 

Imetolewa na:

 

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,

Ikulu,

DAR ES SALAAM.

 

09 Machi, 2010