DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

 

Telephone: 255-22-2114512, 2116898

E-mail: press@ikulu.go.tz             

Fax: 255-22-2113425

 

 

PRESIDENT’S OFFICE,

      THE STATE HOUSE,

       P.O. BOX 9120,  

DAR ES SALAAM.

Tanzania.

 

 

 

 

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

 

Serikali ya Awamu ya Nne imedhamilia kuendeleza kwa dhati hazina ya mradi wa Makaa ya Mawe ya Mchuchuma na yale ya Liganga kwa ajili ya kuendeleza na kuleta maendeleo kwa wananchi.  Rais Jakaya Mrisho Kikwete amewaambia wananchi wa Ludewa katika mkutano wa hadhara uliofanyika leo katika uwanja wa mpira

sabasaba.

 

Dhamira yetu ni kuyaendeleza madini haya na baada ya muda mfupi tutatoa taarifa ya maamuzi yetu ya jinsi ya kuendeleza madini haya”.  Rais amesema

 

            Rais amesema kuendelezwa kwa Linganga na Mchuchuma ni moja ya ahadi za Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi iliyoitoa wakati wa uchaguzi mwaka 2005.

 

            Rais Kikwete amewaeleza wananchi kwamba kazi ya utafiti katika makaa ya mawe ya Mchuchuma imeshakamilika hata hivyo yale ya Liganga bado utafiti unahitajika zaidi na serikali inatafuta namna ya kuharakisha tafiti hizo.  Ili kuendeleza raslimali hizi zenye uwezo mkubwa wa kusukuma maendeleo katika mikoa ya kusini.

 

            Tulichoamua ni kutafuta njia ya haraka ya kutuwezesha kufanikisha miradi hii”.  Rais ameeleza  

 

           Tatizo kubwa katika mradi wa makaa ya mawe ya mchuchuma ni namna gani makaa hayo yatakapochimbwa yataweza kusafirishwa na kufikishwa kwenye soko.  Njia kubwa na inayofaa zaidi ni njia ya reli ambayo ni gharama kubwa sana. Lakini Rais Kikwete amesema pamoja na gharama hizo dhamira kubwa ya serikali yake ni kuyaendeleza madini hayo ili yaweze kuleta maendeleo na baada ya muda mfupi serikali itatoa maamuzi kamili ya miradi hii.

 

          Rais Kikwete yuko mkoani Iringa katika shughuli za kikazi za kukagua maendeleo na kusikiliza matatizo ya wananchi. Mapema leo asubuhi Rais Kikwete ametembelea na kukagua maaka ya mawe ya Mchuchuma na kutembelea kituo cha Umeme cha Ludewa ambacho kimeaanza kutoa umeme kwa wananchi wa mji wa Ludewa na kuona maendeleo ya miradi hii.  Kaitka kituo cha Umeme cha Ludema Rais ameona machine iliyotolewa na kanisa Katoliki na kuwaeleza wananchi kwamba tayari serikali imeangiza machine 2 nyingine kubwa zitakazokuwa na uwezo wa kutoa kilowatt 600 kila moja ambazo zitafungwa na kuongeza umeme katika mji wa Ludewa.

 

Rais Kikwete mchana huu anaelekea wilaya ya Njombe.  Akiwa wilayani humo ataendelea na shughuli za kikazi za kukagua maendeleo na kuzungumza na wananchi.

 

 

Mwisho

Imetolewa na Premi Kibanga

Ludewa

02 Agosti, 2008