DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

 

Telephone: 255-22-2114512, 2116898

E-mail: press@ikulu.go.tz             

Fax: 255-22-2113425

 

Coat of Arms

 

PRESIDENT’S OFFICE,

      THE STATE HOUSE,

       P.O. BOX 9120,  

DAR ES SALAAM.

Tanzania.

 

 

 

 

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI



Serikali ya Awamu ya Nne inalipa uzito mkubwa suala la kilimo, na juhudi sasa zinafanyika kuongeza kasi ya utekelezaji.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete amesema leo wakati akihutubia mkutano wa hadhara huko Lituhi wilayani Mbinga.

Rais amesema Serikali yake imeongeza mbolea ya ruzuku toka bil.7 mwaka 2005 hadi kufika bil.118 mwaka huu.

Akizungumzia juhudi za Serikali katika kuendeleza kilimo wilayani Mbinga Rais amesema mkoa wa Ruvuma utapatiwa matrekta ya mkono 251 na kati ya hayo 50 yatatolewa wilaya ya Mbinga na kipaumbele itakuwa kwenye SACCOS za kilimo.

“Tutatilia mkazo Kilimo cha Umwagiliaji na Matrekta na tayari mil.45 zimewekwa katika akaunti ya wilaya yenu kwa ajili ya matayarisho ya mradi mkubwa wa umwagiliaji.”  Ameelezea.

Mapema leo asubuhi Rais amefungua Mradi wa Maji wa Jamii katika kijiji cha Litumba Kuhamba wenye gharama ya shilingi milioni 210 uliogharamiwa kwa pamoja na wanannchi, Serikali Kuu na Halmashauri ya Wilaya.

Rais pia amekagua kivuko cha Mto  Ruhuhu na kukagua kituo cha Afya cha Lituhi.

Rais amewapongeza wananchi wa Litumba Kuhamba kwa mradi wao wa maji na kuwaeleza kuwa tatizo la maji ni moja ya kero kubwa alizoambiwa wakati wa kampeni na sasa ahadi yake ya kutatua kero hiyo imetimia.

“Wilaya ya Mbinga ilikuwa na tatizo kubwa la maji tumeamua kulitatua na bado mipango inaendelea kutafuta jawabu la kudumu, hii ni awamu ya kwanza, imeisha, awamu wa pili inakuja”.  Amesema, na kueleza kuwa nia ni kuondoa tatizo la maji kabisa.


Mwisho.

Imetolewa na Premi Kibanga,
Songea.
11 Agosti, 2009