DIRECTORATE
OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
UNITED
REPUBLIC OF TANZANIA
|
Telephone:
255-22-2114512, 2116898 E-mail: ikulumawasiliano@yahoo.com Fax: 255-22-2113425
|
|
PRESIDENT’S
OFFICE, THE STATE HOUSE, P.O. BOX
9120, DAR ES SALAAM. Tanzania. |
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Serikali ya Chama Cha
Mapinduzi ina azma ya kuwapatia wananchi wake wote maji safi na salama ifikapo
mwaka 2025.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete amewambia wananchi wa Mugumu, mkoani Mara leo
mchana wakati alipokuwa akiwahutubia baada ya kuzindua bwawa la Manchira
na Kioski cha Maji cha Mugumu.
"Suala la maji ni moja ya vipaumbele vya Chama Cha Mapinduzi, ifikapo mwaka 2025, kila Mtanzania apate maji
safi na salama mita 400 toka alipo na utekelezaji wake unaanza sasa"
Rais amesema.
Amesema Serikali imeongeza bajeti ya maji kwa sababu ya shabaha hiyo mbali na
Maji vipaumbele vingine ni Elimu, Miundombinu, Afya na Kilimo.
Bwawa la Mugumu limegharimu Serikali
shilingi billioni 10.2 na ni moja ya ahadi za Chama Cha Mapinduzi kwa wananchi
wa Mara ya mwaka 2005.
Mji wa Mugumu umekua na tatizo la maji kwa muda mrefu ambapo juhudi za kujenga
Bwawa la Mugumu zilianza miaka 30 iliyopita wakati Rais Kikwete akiwa Waziri wa
Maji.
Ahadi zingine kwa wananchi wa mugumu zilikuwa Umeme ambao tayari umepatikana,
Bwawa la Mugumu ambalo leo limezinduliwa, hospitali ambayo ujenzi umeanza na
barabara na kiwanja cha ndege cha kimataifa ambapo Rais amesema ahadi hii iko
palepale.
Rais amesema barabara hiyo itajengwa katika maeneo ya watu na wala sio ndani ya
hifadhi kama watu wengine wanavyosema.
"Kilomita 50 ndani ya hifadhi hazitawekwa lami lakin lami itawekwa nje
ya hifadhi kwa wananchi ili tusiwanyime haki ya uchumi wao kuendelea".
Amefafanua
Rais pia amedokeza nia ya Serikali ya Chama Cha Mapinduzi kujenga Chuo Kikuu
kingine mkoani Mara ili kupanua fursa za Elimu Nchi.
"Kuanzia 2015-20 mtoto wa Tanzania akianza shule lazima afike Form Four
na mipango hiyo ina anza sasa na ndiyo sababu elimu itaendelea kuwa kipaumbele
cha mwanzo kwa muda mrefu" Rais amewaeleza wananchi na kuwataka
walinde vyanzo vya maji, watunze Bwawa na kuchangia gharama kwani Bwawa limeishakabidhiwa
kwao.
Mwisho.
Imetolewa na Premi Kibanga,
MUGUMU,
Mara.
02 Julai, 2010