UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

 

Telephone: 255-22-2114512, 2116539

E-mail: press@ikulu.go.tz

Website:  www.mawasilianoikulu.go.tz  

Fax: 255-22-2113425

 

Coat of Arms

 

PRESIDENT’S OFFICE,

      THE STATE HOUSE,

       P.O. BOX 9120,  

DAR ES SALAAM.

Tanzania.

 

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Tanzania bado inaamini na kusimamia misingi na imani ile ile iliyokuwa nayo miaka hamsini nyuma, juu ya Umoja wa Mataifa kama ilivyoainishwa na waasisi wa taifa letu.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete amesema hayo wakati wa kutuhutubia Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa  (UN) jijini New York Marekani, jana tarehe  22 Septemba, 2011.

Najivunia kuwa Tanzania inaendelea kuamini misingi ya UNO, na mwanachama hai wa baraza hili la Dunia, tunaahidi kuendelea kuamini hivyo kwa miaka mingine 50 na zaidiAmeeleza .

Rais ameeleza kuwa katika miaka hiyo 50 ya uanachama wa Umoja wa Mataifa, Tanzania imeshiriki katika shughuli za kulinda Amani na Usalama Barani Afrika na sehemu nyinginezo duniani kama ilivyotakiwa kufanya hivyo na UN.

Siku zote tumekuwa tukiamini kuwa mazungumzo, kuzuia na usuluhishi wa migogoro  ndiyo njia sahihi zaidi ya ya kutatua migogoro.  Hivyo, Tanzania imekuwa siku zote mstari wa mbele katika kuongoza mazungumzo ya kutatua migogoro katika nchi zinazotuzunguka, katika kanda yetu na kwingineko Barani Afrika”.  Ameeleza.

Tanzania imekuwa mstari wa mbele katika kuchangia katika shughuli hizo kwa kutuma polisi, jeshi na hata rai wa Nyanja mbalimbali katika shughuli za amani za UN na pia pamoja na Denmark mwaka 2006, zimefanikiwa kuongoza katika kuundwa kwa Kamisheni ya Amani.

Katika hotuba yake, Rais Kikwete amewakumbusha wajumbe jinsi Baba wa Taifa, Hayati Julius Kambarage Nyerere alivyokataa na kupinga ukoloni na ubaguzi wa aina yeyote ile Barani Afrika na duniani kote na kusema kuwa Uhuru wa nchi yetu haungeweza kukamilika mpaka nchi zingine zote Afrika zimekuwa huru.

Na ndipo akaazimia kuzisaidia nchi zingine katika harakati za ukombozi na hatimaye uhuru wa nchi hizo.

Kama tulivyokuwa na amini wakati wa uhuru, bado tunaamini leo kuwa binadamu wote ni sawa na wanastahili haki zote na kulindwa na kuheshimiwa haki zao za kiraia, kisiasa, kiuchumi, kijamii na kitamaduni  kama inavyoanishwa katika mkataba wa kimataifa wa haki za binadamu”. Rais amesisitiza na kusisitiza kuunga mkono jitihada za watu wa Palestina katika harakati zao za kutafuta uhuru wao.

Amesema Tanzania ingependa kuona nchi mbili za Israeli na nchi huru ya kidemokrasia ya Palestina wakiishi kwa amani na utulivu na katika misingi ile ile Tanzania inaunga mkono jitihada za watu wa Cuba kutaka vikwazo vyote viondoshwe dhidi yao.

Watu hawa katika nchi hizi mbili wameteseka kwa muda mrefu  na umefika sasa wakati kwa mzigo huu uondoshwe kutoka mabegani mwao”.  Rais amesema.

Rais ameendelea na mikutano na viongozi mbalimbali duniani na wawekezaji ambao wana biashara zao nchini Tanzania na wale wanaotaka kuwekeza Tanzania.

Mwisho.

Imetolewa na Premi kibanga,

Mwandishi wa Habari wa RaisMsaidizi,

New York.

Marekani.

23 Septemba, 2011