DIRECTORATE
OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
UNITED
|
Telephone: 255-22-2114512, 2116898 E-mail: ikulumawasiliano@yahoo.com Fax: 255-22-2113425
|
|
PRESIDENT’S OFFICE, THE
STATE HOUSE, P.O. BOX 9120, DAR
ES SALAAM. Tanzania. |
TAARIFA
KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais
Jakaya Mrisho Kikwete ameondoka leo mchana kuelekea
Kampala Uganda kuhudhuria kikao cha 15 cha Baraza Viongozi wa Umoja wa Afrika
(AU) kinachoanza leo 25 Julai hadi 27 mwezi
huu.
Mada
kuu ya mkutano
huo ni
Afya ya Mama na Mtoto na
Maendeleo Afrika
Mbali
na ajenda hiyo kikao cha viongozi kitajadili mabadiliko kuhusu kamisheni ya Umoja
wa Afrika kuwa Mamlaka ya
Umoja wa Afrika (Transformation
of the African Union(AU) into the African Union
Authority(AUA).
Pamoja na
hayo kIkao kinatarajia kuteua Majaji wa Mahakama
ya Afrika ya Haki za
Binadamu na uteuzi wa wana
kamati ya Haki za Mtoto
na kujadili ripoti ya Baraza
la Amani na Usalama kuhusu Afrika.
Mada inayohusu Afya ya Mama na Mtoto ni muhimu Barani
Afrika na inategemewa kwamba itatoa nafasi kwa
wakuu wa nchi hizi kudhibitisha
msimamo wao wa kisiasa na
pia kuboresha hali ya Afya
ya Mama. Na mtoto barani.
Kesho tarehe 26 Julai Rais Kikwete
anatarajiwa kuongoza viongozi wa Afrika
waliokatika ushirikiano wa kupambana na
Malaria barani , African Leaders
Malaria Alliance (ALMA).
Ushirikiano wa viongozi chini ya ALMA ulianzishwa mwezi Sepemba, 2009 katika kikao kilichofanyika chini ya Uenyekiti
wa Rais Kikwete
ambapo nchi 22 ziliafiki kuundwa kwa ushirikiano huo na mpaka
leo nchi 28 zimeshajiunga.
Rais Kikwete anatarajia kurejea mara baada
ya mkutano kumalizika tarehe 27 Julai, 2010.
Mwisho
Imetolewa
na:
Kurugenzi
ya Mawasiliano,
Ikulu,
Dar
es Salaam.
25
Julai, 2010