DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL
COMMUNICATIONS
UNITED
|
Telephone: 255-22-2114512, 2116898 E-mail: ikulumawasiliano@yahoo.com Fax: 255-22-2113425
|
|
PRESIDENT’S OFFICE,
THE STATE HOUSE, P.O. BOX 9120, DAR ES SALAAM. Tanzania. |
TAARIFA
KWA VYOMBO VYA HABARI
Tanzania
ni moja
ya nchi nne
(4) za kwanza duniani zinazotarajia kunufaika na uhusiano wake mzuri na Marekani.
Naibu
Waziri wa Nchi wa Marekani
anayeshughulikia Masuala ya Afrika, Bw.
Johnie Carson amemweleza Rais Kikwete alipofika
Ikulu leo
mchana ambapo ameleta salaam za Rais Obama na kueleza
mpango mpya wa Marekani wa
kuongeza kasi ya ushirikiano baina ya Marekani
na nchi mbalimbali
duniani.
“Marekani inataka kuongeza mazungumzo na uhusiano na
nchi mbalimbali duniani, na Tanzania ni moja ya
wenza wetu katika maendeleo, na tunaiona Tanzania kuwa ni moja
ya wenza madhubuti katika mazungumzo na tunataka kushirikiana
zaidi na Tanzania” Bw. Carson amesema.
Katika
ushirikiano huo mpya nchi za
Ufilipino, El Salvador, Tanzania na Ghana zitashirikiana na Marekani ambapo
uhusiano huo mpya una lengo
la kufanya mazungumzo ya pamoja ambayo
yataharakisha maendeleo na kuleta maendeleo
katika nchi hizi.
“Marekani inajivunia uhusiano huu kwa sababu Tanzania imetekeleza na kutumia misaada ya Marekani vizuri
na hivyo tunataka tushirikiane zaidi”Amesema.
Bwana
Carson yuko nchini na ujumbe
wa wataalamu ambao watakaa na
wataalamu na viongozi wa Serikali
ya Tanzania na kwa pamoja watabainisha
maeneo ambayo yatafanyiwa kazi na hatimaye kuongeza
kasi ya maendeleo.
Mazungumzo
hayo yataangalia sekta mbalimbali za kilimo, biashara,
miundo mbinu na maeneo
mengine ya maendeleo.
Rais
Kikwete amemhakikishia Naibu Waziri huyo
wa Marekani
kuwa Tanzania imepania kuleta maendeleo kwa wananchi wake na misaada yote
ya Serikali ya Marekani imekuwa
ya manufaa na yenye kugusa
maslahi ya wananchi.
“Tanzania
imefaidika sana na uhusiano huu,
misaada ya Mrekani kwenye malaria, HIV, barabara, maji, kilimo na sasa
uhusiano huu mpya, yote haya
ni mambo mazuri na yenye manufaa
kwa wananchi wake” amesisitiza na kuongeza kuwa
uhusiano huo mpya, umeongeza matumaini mapya katika juhudi za
Serikali ya Awamu ya Nne
kuleta maendeleo na kukuza uchumi.
Mwisho.
Imetolewa
na Premi
Kibanga,
Mwandishi
wa Habari
wa Rais Msaidizi,
Ikulu.
Dar
es Salaam.
8
Februari, 2011