DIRECTORATE
OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
UNITED
|
Telephone: 255-22-2114512, 2116898 E-mail: ikulumawasiliano@yahoo.com Fax: 255-22-2113425
|
|
PRESIDENT’S OFFICE, THE
STATE HOUSE, P.O. BOX 9120, DAR
ES SALAAM. Tanzania. |
TAARIFA
KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais Jakaya
Kikwete amepanda miti katika maeneo ambayo patasimikwa mitambo ya
kuzalisha umeme katika wilaya za Kasulu na Kibondo Mkoani Kigoma.
"Mkoa wa Kigoma umekuwa na matatizo ya umeme kwa muda mrefu tuaminiane,
tuvumiliane ahadi yetu iko pale pale, kumaliza tatizo la umeme Kasulu na
Kibondo" Rais amewambia wananchi wa Kasulu jana (16/06/2010)
wakati wa ziara ya kikazi katika wilaya hizo mbili ambapo yuko kwa shughuli za
kukagua maendeleo na kuona hatua zilizofikiwa katika kutatua kero mbalimbali za
wananchi Mkoani Kigoma.
Mitambo hiyo miwili, kila mmoja una uwezo wa kuzalisha megawati mbili na nusu
na inategemewa kuanza uzalishaji mwishoni mwa mwaka huu.
Katika ahadi yake hiyo ya kufikisha umeme katika makao makuu ya wilaya,
itatimizwa pia katika wilaya za Bukombe, Longido, Nkasi, Nanyumbu, Namtumbo
na Ngorongoro.
Zote hizi zitapewa huduma ya umeme ndani ya bajeti hii ambayo ni ya mwisho
kabla ya kufanyika tena kwa uchaguzi mkuu nchini.
Rais amewambia wananchi wa Kasulu kuwa serikali pia imedhamiria kuzalisha umeme
kutoka Mto Malagalasi ambao utaongezea katika mahitaji mkoani humo hadi katika
vijiji.
Miradi ya umeme katika mikoa hii miwili inafadhiliwa na fedha za serikali
ambapo mradi wa Kasulu umegharimu Tshs Bil 7.2 na wa Kibondo shilingi Bil 7.9
ambapo mkandarasi ameanza kupeleka vifaa kwenye eneo.
Rais Kikwete amesema kero hizi kubwa zimefanya wananchi wa Kigoma kuona kuwa
wametengwa. Rais Kikwete pia amefanya
ukaguzi wa ujenzi wa barabara unaoendelea mkoani humu ambapo amewaeleza
wananchi wa Kasulu kuwa mbali na kuunganisha mikoa yote nchini kwa barabara za
lami, serikali pia itaunganisha nchi yetu na nchi jirani kwa barabara za lami.
"Mwaka huu wa fedha ujenzi wa barabara utaendelea hadi Kasulu na mwakani
tutaenda hadi Kibondo”. Rais amesisitiza.
Ahadi zingine kwa mkoa wa Kigoma ni utatuzi wa kero za maji na Rais amezindua
mradi wa maji wa Mkongoro II.
Rais anamalizia ziara yake ya kikazi ya siku tatu mkoani kigoma leo tare 17 Juni,
2010 na kuelekea Wilaya ya Mpanda, mkoani Rukwa.
Mwisho.
Imetolewa
na Premi Kibanga,
Mwandishi
wa Habari Msaidizi wa Rais,
Safarini Kigoma.
17
Juni, 2010