PRESS SECRETARY TO THE PRESIDENT OF THE
UNITED
The State House,
Tel:
Fax. No. 255-22 2113425 DAR ES SALAAM.
E-mail: press@ikulu.go.tz TANZANIA.
ikulupress@yahoo.com
TAARIFA
KWA VYOMBO VYA HABARI
Premi Kibanga,
Bariadi,
27. Aug, 07.
Mbunge wa
Bariadi Mashariki Mhe. John Cheyo amempongeza Rais Jakaya Mrisho Kikwete
kwa kutimiza
ahadi aliyoitoa kwa wananchi wa
jimbo
“Wewe ni
Rais unayetimiza ahadi zako,ulituahidi kujenga daraja mto Simiyu nakushukuru
kwa hilo fedha zimekuja na mhandisi ameanza
kazi, ulituahidi kutusaidia swala la bei ya pamba,
kwa mara ya kwanza mwaka huu bei imekuwa
nzuri sana na wananchi wameongeza
juhudi katika kulima pamba, tunaomba
utusaidie isishuke tena, Mheshimiwa Urais wako una
baraka sana, nakushukuru kwa hilo” amesema Mheshimiwa
Cheyo.
Rais Kikwete amefika Bariadi leo na kuanza
shughuli zake za kukagua miradi
ya maendeleo na
utekelezaji wa ahadi zake za
uchaguzi kwa kuzindua bwawa la maji la Mwalushu lililobomoka kufuatia mvua nyingi
zi.lizonyesha mwaka 2000.
Bwawa
Akijibu shukrani hizo za Mheshimiwa
Cheyo, Rais ameahidi kushirikiana na wananchi
hao katika shughuli za maendeleo
bila ubaguzi.
“Tunao wajibu
kuwatumikia wananchi hata
Rais amewahimiza wananchi wa
Bariadi kufuata kanuni kuu za
ulimaji wa Pamba ili kufikia
lengo la taifa la kupata kilo elfu moja kwa eka
kutoka kilo mia tatu za sasa.
“Kilio chenu kingine kilikuwa
pamba, jitihada zinafanyika kuhakikisha bei haishuki bali
inaimarika zaidi, nanyi zingatieni kanuni’. Amesema Rais.
Rais ameingia wilayani Bariadi kukamilisha ziara ya mkoa wa Shinyanga kabla ya kufanya
majumuisho.
Mwisho.