DIRECTORATE
OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
UNITED
|
Telephone: 255-22-2114512, 2116898 E-mail: ikulumawasiliano@yahoo.com Fax: 255-22-2113425
|
|
PRESIDENT’S OFFICE, THE
STATE HOUSE, P.O. BOX 9120, DAR
ES SALAAM. Tanzania. |
TAARIFA
KWA VYOMBO VYA HABARI
Miradi ya maendeleo iliyokubaliwa kati ya
Balozi wa Marekani Alfonso Lenhardt
amemueleza Rais Jakaya Mrisho Kikwete leo asubuhi (Machi 25, 2010) alipofika
Ikulu kumpa taarifa ya maendeleo ya makubaliano hayo ambapo kiasi cha Dola
milioni 698 zimetolewa na Marekani kwa
Miradi hiyo ni ya barabara, Nishati na Maji
ambapo tayari mjenzi wa barabara ya Tanga - Horohoro yuko katika eneo la
ujenzi, Laela -Sumbawanga, Songea - Namtumbo ambazo uchambuzi wa zabuni umeshaanza na wakandarasi
wanatarajiwa kuteuliwa Mwezi April,
20010.
Miradi mingine ni Tunduma – Ikana - Laela
na Peramiho - Mbinga ambapo taratibu za zabuni zimeanza na zoezi la uchambuzi
litaanza mwezi ujao.
Katika mradi wa Pemba, tayari nyaraka za
zabuni zinatayarishwa na taratibu za fidia kwa wananchi zimeanza kuchambuliwa.
Katika miradi ya Nishati, mradi wa
kusambaza umeme (Zanzibar Cable) taratibu zimeshafanyika na inatarajiwa kwamba
shughuli ya kutiliana saini kati ya mkandarasi na serikali itafanyika mwezi
ujao.
Katika mradi wa usambazaji wa Umeme katika
mikoa 6 ya Tanzania Bara, taratibu za kumpata mzabuni zimeshaanza ambapo mikoa ya
Balozi Lenhardt alikuwa ameambatana na
Mkurugenzi Mwakilishi hapa Tanzania Bw.
Karl Fickenscher ambapo pia amemueleza Rais Kikwete kuwa miradi ya maji ya Ruvu
Chini na mkoani Morogoro, wajenzi
wameshaanza kuorodheshwa na zoezi la kuandaa zabuni limeanza
Katika kikao hicho balozi Lenhardt
amemueleza kuwa kufuatia Mazungumzo kati ya Rais Kikwete na Rais Obama mwaka
jana, Marekani imeiteua
Balozi pia amemueleza Rais Kikwete kuwa
Marekani itatoa msaada wa ujenzi na ukarabati wa Reli ya Kati, Rais Kikwete
amefurahishwa na msaada huo ambapo ameelezea kuwa huo ni mchango mkubwa kwa maendeleo
na uchumi wa Tanzania kwani reli yetu kwa sasa ni ya zamani na finyu sana. Kufuatia
msaada huu, mazungumzo kati ya serikali ya
Katika mazungumzo hayo Marekani pia
itaendeleza programu yake ya kuisaidia
Akielezea kuhusu mpango huo, Mkurugenzi wa
Shirika la Misaada la Marekani (USAID)
hapa nchini Bwana Robert Cunnane amesema USAID itashirikiana na Wizara ya Afya
nchini ili kuelekeza msaada huo katika jitihada za kitaifa za kupambana na
Ukimwi.
Marekani imekuwa mstari wa mbele katika
kuisaidia
Mambo mengine yaliyojadiliwa katika kikao
hicho ni msaada kutoka marekani katika kupambana na maharamia katika bahari ya
Hindi na kutoa msaada wa utaalamu na stadi za kuchimba na kuendeleza madini ya
uranium hapa nchini ambayo yamegunduliwa huko kusini mwa
Imetolewa
na:
Premi
Kibanga,
Mwandishi
wa Habari wa Rais Msaidizi,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
25
March, 2010